< 1 Kings 13 >

1 And, behold, there came a man of God out of Judah by the word of the LORD unto Beth-el; and Jeroboam was standing by the altar to offer.
Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
2 And he cried against the altar by the word of the LORD, and said: 'O altar, altar, thus saith the LORD: Behold, a son shall be born unto the house of David, Josiah by name; and upon thee shall he sacrifice the priests of the high places that offer upon thee, and men's bones shall they burn upon thee.'
Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
3 And he gave a sign the same day saying: 'This is the sign which the LORD hath spoken: Behold, the altar shall be rent, and the ashes that are upon it shall be poured out.'
Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
4 And it came to pass, when the king heard the saying of the man of God, which he cried against the altar in Beth-el, that Jeroboam put forth his hand from the altar, saying: 'Lay hold on him.' And his hand, which he put forth against him, dried up, so that he could not draw it back to him.
Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
5 The altar also was rent, and the ashes poured out from the altar, according to the sign which the man of God had given by the word of the LORD.
Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
6 And the king answered and said unto the man of God: 'Entreat now the favour of the LORD thy God, and pray for me, that my hand may be restored me.' And the man of God entreated the LORD, and the king's hand was restored him, and became as it was before.
Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
7 And the king said unto the man of God: 'Come home with me, and refresh thyself, and I will give thee a reward.'
Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 And the man of God said unto the king: 'If thou wilt give me half thy house, I will not go in with thee, neither will I eat bread nor drink water in this place.
Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
9 For it so was charged me by the word of the LORD, saying: Thou shalt eat no bread, nor drink water, neither return by the way that thou camest.'
kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
10 So he went another way, and returned not by the way that he came to Beth-el.
Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
11 Now there dwelt an old prophet in Beth-el; and one of his sons came and told him all the works that the man of God had done that day in Beth-el, and the words which he had spoken unto the king, and they told them unto their father.
Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
12 And their father said unto them: 'What way went he?' For his sons had seen what way the man of God went, that came from Judah.
Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
13 And he said unto his sons: 'Saddle me the ass.' So they saddled him the ass; and he rode thereon.
Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
14 And he went after the man of God, and found him sitting under a terebinth; and he said unto him: 'Art thou the man of God that camest from Judah?' And he said: 'I am.'
Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Then he said unto him: 'Come home with me, and eat bread.'
Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
16 And he said: 'I may not return with thee, nor go in with thee; neither will I eat bread nor drink water with thee in this place.
Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
17 For it was said to me by the word of the LORD: Thou shalt eat no bread nor drink water there, nor turn back to go by the way that thou camest.'
kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
18 And he said unto him: 'I also am a prophet as thou art; and an angel spoke unto me by the word of the LORD, saying: Bring him back with thee into thy house, that he may eat bread and drink water.' — He lied unto him. —
Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
19 So he went back with him, and did eat bread in his house, and drank water.
Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
20 And it came to pass, as they sat at the table, that the word of the LORD came unto the prophet that brought him back.
Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
21 And he cried unto the man of God that came from Judah, saying: 'Thus saith the LORD: Forasmuch as thou hast rebelled against the word of the LORD, and hast not kept the commandment which the LORD thy God commanded thee,
naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
22 but camest back, and hast eaten bread and drunk water in the place of which He said to thee: Eat no bread, and drink no water; thy carcass shall not come unto the sepulchre of thy fathers.'
bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
23 And it came to pass, after he had eaten bread, and after he had drunk, that he saddled for him the ass, namely, for the prophet whom he had brought back.
Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
24 And when he was gone, a lion met him by the way, and slew him; and his carcass was cast in the way, and the ass stood by it; the lion also stood by the carcass.
Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
25 And, behold, men passed by, and saw the carcass cast in the way, and the lion standing by the carcass; and they came and told it in the city where the old prophet dwelt.
Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
26 And when the prophet that brought him back from the way heard thereof, he said: 'It is the man of God, who rebelled against the word of the LORD; therefore the LORD hath delivered him unto the lion, which hath torn him, and slain him, according to the word of the LORD, which He spoke unto him.'
Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
27 And he spoke to his sons, saying: 'Saddle me the ass.' And they saddled it.
Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
28 And he went and found his carcass cast in the way, and the ass and the lion standing by the carcass; the lion had not eaten the carcass, nor torn the ass.
Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
29 And the prophet took up the carcass of the man of God, and laid it upon the ass, and brought it back; and he came to the city of the old prophet, to lament, and to bury him.
Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
30 And he laid his carcass in his own grave; and they made lamentation for him: 'Alas, my brother!'
Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
31 And it came to pass, after he had buried him, that he spoke to his sons, saying: 'When I am dead, then bury me in the sepulchre wherein the man of God is buried; lay my bones beside his bones.
Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
32 For the saying which he cried by the word of the LORD against the altar in Beth-el, and against all the houses of the high places which are in the cities of Samaria, shall surely come to pass.'
Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
33 After this thing Jeroboam returned not from his evil way, but made again from among all the people priests of the high places; whosoever would, he consecrated him, that he might be one of the priests of the high places.
Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
34 And by this thing there was sin unto the house of Jeroboam, even to cut it off, and to destroy it from off the face of the earth.
Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.

< 1 Kings 13 >