< Revelation 5 >

1 AND I saw on the right hand of him who was seated on the throne a volume of a book written within, and on the back sealed with seven seals.
Kisha nikaona katika mkono wa kulia wa yule aliyekuwa amekaa katika kiti cha enzi, gombo lililoandikwa mbele na nyuma, na lilikuwa limetiwa mihuri saba.
2 And I saw mighty angel proclaiming with a loud voice, Who is worthy to open the book, and to break the seals thereon?
Nilimwona malaika mwenye nguvu akihubiri kwa sauti kubwa, “Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?”
3 And no man was able in heaven, nor upon earth, nor under the earth, to open the book, nor to look into it.
Hakuna mtu mbinguni au duniani au chini ya dunia aliyeweza kulifungua gombo au kulisoma.
4 And I wept much because no man was found worthy either to open or read the book, or even to look upon it.
Nililia kwa uchungu kwa kuwa hakupatikana yeyote aliyestahili kulifungua gombo au kulisoma.
5 And one of the presbyters said unto me, Weep not: behold the lion who is of the tribe of Judah, the root of David, hath prevailed, to open the book, and to break the seven seals upon it.
Lakini mmoja wa wazee akaniambia, “Usilie. Tazama! Simba wa kabila ya Yuda, shina la Daudi, ameshinda, na anaweza kulifungua gombo na mihuri yake saba.”
6 And I beheld, and lo! in the midst of the throne, and of the four living beings, and in the midst of the presbyters, stood a lamb as just slaughtered, having seven horns and seven eyes, which are the seven spirits of God that are sent forth into all the world:
Kati ya kiti cha enzi na wenye uhai wanne na miongoni mwa wazee, niliona mwanakondoo amesimama, akionekana kama aliye uawa. Alikuwa na pembe saba na macho saba - hizi ni roho saba za Mungu zilizotumwa duniani kote.
7 and he came and took the book out of the right hand of him that was seated upon the throne.
Akaenda akalichukua gombo kutoka katika mkono wa kuume wa yule aliye kaa katika kiti cha enzi.
8 And when he had taken the book, the four living beings and the four and twenty presbyters prostrated themselves before the lamb, having each harps, and vases of gold, full of perfumes smoaking, which are the prayers of the saints.
Alipolichukua gombo, wenye uhai wanne na wazee ishirini na wanne wakainama hadi nchi mbele ya mwanakondoo. Kila mmoja alikuwa na kinubi na bakuli ya dhahabu iliyojaa uvumba ambayo ni maombi ya waamini.
9 And they sung a new song, saying, Worthy art thou to take the book, and to open the seals thereon; because thou hast been slaughtered, and hast redeemed us for God by thy blood, out of every tribe, and tongue, and people, and nation;
Waliimba wimbo mpya: “Unastahili kulitwaa gombo na kuzifungua muhuri zake. Kwa kuwa ulichinjwa, na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu wa kila kabila, lugha, jamaa na taifa.
10 and hast made us for our God kings and priests, and we shall reign upon the earth.
Ukawafanya ufalme na makuhani kwa ajili ya kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala juu ya nchi.”
11 And I looked, and heard the voice of many angels around the throne, and the living beings, and the presbyters, and their number was myriads of myriads and thousands of thousands,
Kisha nilitazama na nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kiti cha enzi - idadi yao ilikuwa 200, 000, 000 na wenye uhai na wazee.
12 crying with a loud voice, Worthy is the slaughtered lamb to receive power, and riches, and wisdom, and might, and honour, and glory, and blessing.
Wakasema kwa sauti kuu, “Astahili mwanakondoo ambaye amechinjwa kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, heshima, utukufu, na sifa.”
13 And every creature which is in heaven, and on the earth, and under the earth, and those who are on the sea, and all things which are therein, heard I, saying, To him who is seated on the throne, and to the lamb, be blessing, and honour, and glory, and might for ever and ever. (aiōn g165)
Nikasikia kila kilichoumbwa kilichokuwa mbinguni na duniani na chini ya nchi na juu ya bahari, kila kitu ndani yake kikisema, “Kwake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi na kwa mwanakondoo, kuwe sifa, heshima, utukufu na nguvu ya kutawala milele na milele.” (aiōn g165)
14 And the four living beings said, Amen. And the four and twenty presbyters prostrated themselves, and worshipped him that liveth for ever and ever.
Wenye uhai wanne wakasema, “Amina!” na wazee wakainama chini na kuabudu.

< Revelation 5 >