< Luke 12 >
1 MEANTIME myriads of people collecting, so that they trod on one another, he began to speak to his disciples, Take heed principally of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy.
Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2 For there is nothing concealed, that shall not be laid open; nor hid, which shall not be known.
Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3 Wherefore whatsoever things ye have spoken in darkness, they shall be reported in the light; and what ye have whispered into the ear in the closets, shall be proclaimed on the house-tops.
Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4 But I say to you my friends, Be not afraid of those who may kill the body, but after that, have nothing farther which they can do.
“Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5 But I will point out to you, whom ye should fear: Fear him, who, after he hath killed, hath power to cast into hell; yea, I say unto you, Fear him! (Geenna )
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna )
6 Are not five sparrows sold for two farthings, yet not one of them is forgotten before God?
Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7 But even the hairs of your head are all numbered: fear not then, ye are of more value than many sparrows.
Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8 But I tell you, Every one who shall confess me before men, him will the Son of man also confess before the angels of God:
“Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9 but he that disowns me before men, shall be disowned before the angels of God.
Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10 And every one who shall utter a word against the Son of man, it shall be forgiven him; but for him who hath blasphemed against the Holy Ghost, there shall be no forgiveness.
“Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 And when they shall bring you before the synagogues, and magistrates, and the ruling powers, be under no anxiety how or what defence ye shall make, or what ye shall say:
“Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12 for the Holy Ghost will teach you at that very hour what ye ought to say.
Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
13 Then spake one of the multitude to him, Master, order my brother to divide the inheritance with me.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
14 But he said to him, Man, who made me a judge and a divider among you?
Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
15 Then said he to them, Beware, and be on your guard against covetousness; for a man’s life doth not depend on the abundance of his possessions.
Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
16 And he spake a parable unto them, saying, The estate of a certain rich man bore plentifully:
Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17 and he thought within himself, saying, What shall I do? for I have not room where I may house my crops.
Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18 And he said, I will do this; I will take down my barns, and build them larger, and collect there all my crops, and my good things!
Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19 And I will say to my soul, Soul, thou hast a multitude of good things in store for many years, be at ease, eat, drink, and be merry!
Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 But God said to him, Thou fool! this night shall they demand thy life from thee; and the things which thou hast prepared, whose shall they be?
Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
21 Just such is every one who heapeth up treasure for self, and is not rich towards God.
Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
22 Then said he to his disciples, For this reason I tell you, Be under no anxiety about your life, what ye shall eat, nor for your body, how ye shall be clothed.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23 The life is more than food, and the body than raiment.
Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24 Consider the ravens, for they neither sow nor reap; they have neither storehouse nor barn; yet God feedeth them: how much are ye more excellent than the birds?
Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25 Which of you, with all his anxiety, can add one moment to his life?
Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26 If therefore ye are unable to do the least thing, why are ye anxious about the others?
Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27 Observe the lillies how they grow up, they toil not, nor spin; but I tell you, that Solomon in all his glory, was not arrayed like one of these.
Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28 If God then so clothe the grass in the field, which to-day is, and to-morrow is thrown into the furnace; how much more you, O ye of little faith?
Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29 So then be not ye inquisitive what ye shall eat, or what ye shall drink, nor be agitated with restless anxiety.
“Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30 For after all these things are the nations of the world seeking; and your Father knoweth that ye have need of these things.
Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31 But seek ye the kingdom of God, and all these things shall be given you over.
Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32 Fear not, little flock! for your Father takes delight in giving you the kingdom.
“Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33 Sell all your possessions, and give in charity; make yourselves purses that wax not old, a treasure never failing in the heavens, where no thief approaches, nor doth the moth destroy.
Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34 For where your treasure is, there will your heart be also.
Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35 Let your loins be firmly girded round, and your lamps burning:
“Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 and ye like men, expecting their master, when he shall return from the marriage; that when he comes and knocks, they may instantly open the door for him.
muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37 Blessed are those servants, whom the Master, when he cometh, shall find watchful: verily I say unto you, that he will gird up himself, and make them sit down at table, and come and wait upon them.
Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38 And if he come in the second watch, or in the third watch, and find them so watchful, blessed are those servants.
Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39 Now this be assured of, that if the master of the family had known at what hour the thief would come, he would have watched, and would not have suffered his house to be broken through.
Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40 Therefore be ye also ready, for at an hour that ye think not of, the Son of man cometh.
Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
41 Then said Peter unto him, Lord, speakest thou this parable to us, or also for all?
Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
42 And the Lord said, Who indeed is a faithful steward, and prudent, whom the lord will place over his household, to give them their proportion of provision at the proper season?
Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43 Blessed is that servant, whom his lord, when he cometh, shall find so employed.
Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Verily I say unto you, that he will place him over all his property.
Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45 But if that servant say in his heart, My master will be a long while ere he comes; and shall begin to beat the men and maid-servants, and to eat and to drink, and to get drunk;
Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46 the master of that servant will come in a day when he doth not expect him, and at an hour which he knoweth not, and shall cut him asunder, and give him his portion with the unfaithful.
bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47 And that servant, who knew his master’s will, and made no preparation for him, nor did according to his pleasure, shall be beaten with many stripes.
Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48 But he that knew it not, yet did things worthy of stripes, shall be beaten with few. For of every one to whom much is given, much shall be required from him: and to whom men commit much, they will of him demand abundantly more.
Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49 I am come to cast fire on the earth, and what is my wish? that it may be now kindled.
“Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50 But I have a baptism to be baptised with; and how am I distressed in spirit till it is finished!
Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51 Think ye that I came to bring peace upon earth? No, I tell you; but rather division:
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52 for henceforth five shall be in one house, divided, three against two, and two against three.
Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 The father shall take part against the son, and the son against the father; the mother against the daughter, and the daughter against the mother; the step-mother against her daughter-in-law, and the son’s wife against her mother-in-law.
Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Then said he to the multitudes, When ye see a cloud rising from the west, ye say immediately, There cometh a shower; and it is so.
Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55 And when the south wind gently blows, ye say, It will be sultry hot; and so it is.
Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56 Ye hypocrites! ye know how to discern by experience from the appearance of the earth and of the sky; but how is it that ye do not discern this particular time?
Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57 And why even of yourselves do ye not decide what is just?
“Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58 For as thou art going with thy prosecutor to the magistrate, on the way endeavour to make up the matter with him; lest he drag thee before the judge, and the judge deliver thee to the officer, and the officer cast thee into prison.
Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59 I tell thee, thou mayest in no wise come out from thence, until thou hast paid the very last mite.
Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”