< John 7 >
1 AND Jesus after these things travelled about in Galilee: for he would not go about in Judea, because the Jews sought to kill him.
Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
2 And a feast of the Jews was nigh, the feast of tabernacles.
Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
3 Then said his disciples to him, Depart hence, and go into Judea, that thy disciples also may see thy works which thou doest.
Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
4 For no man doeth any thing in secret, yet seeketh himself to appear publicly: if thou doest these things, exhibit thyself to the world.
Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
5 For even his own brethren did not believe on him.
Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
6 Jesus therefore saith to them, My proper time is not yet come: but your time is always ready.
Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
7 The world cannot hate you, but me it hateth, because I testify of it, that its deeds are evil.
Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
8 Go ye up to this feast: for I am not yet going up to this feast, because my fixed time is not yet arrived.
Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
9 Thus speaking to them then, he continued in Galilee.
Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
10 But as soon as his disciples were gone up, then went he also himself up to the feast: not in public, but as in concealment.
Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
11 The Jews then sought for him at the feast, and said, Where is he?
Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
12 And there was a great murmur concerning him among the multitude: some said, Surely he is a good man: others said, No; he only deceiveth the people.
Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
13 Yet no person spake openly of him for fear of the Jews.
Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
14 But now at the middle of the feast Jesus went up into the temple, and taught.
Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
15 And the Jews marvelled, saying, How knoweth this man the scriptures, not being a scholar?
Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
16 Jesus answered them and said, My doctrine is not mine, but his that sent me.
Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17 If any man will do his will, he shall know respecting the doctrine, whether it is of God, or whether I speak from myself.
Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
18 He that speaketh from himself, seeks his own individual honour: but he that seeketh the glory of him that sent him, he is true, and iniquity in him there is none.
Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
19 Hath not Moses given you the law, yet none of you practises the law? Why do ye seek to kill me?
Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
20 The multitude answered and said, Thou hast a devil: who is seeking to kill thee?
Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
21 Jesus answered and said unto them, I have performed one work, and ye all marvel.
Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
22 Because Moses ordered you circumcision; (not that it comes from Moses, but from our ancestors; ) so ye circumcise a man on the sabbath-day.
Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
23 If a man receive circumcision on the sabbath-day, that the law of Moses should not be violated; are ye incensed against me, because I have made a man whole on the sabbath-day?
Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
24 Judge not by appearance, but judge righteous judgment.
Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
25 Then said some of the people of Jerusalem, is not this the man whom they are seeking to kill?
Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
26 And, lo! he speaketh openly, and they say not a word to him. Do the rulers certainly know that this man is really the Messiah?
Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
27 But we know this man whence he is: but when the Messiah cometh, no man knoweth whence he is.
Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
28 Then spake Jesus aloud as he was teaching in the temple, and said, Ye both know me, and ye know from whence I am: and I came not of myself, but he that sent me is true, whom ye know not.
Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
29 But I know him: for I am from him, and he hath sent me.
Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
30 Then they sought to apprehend him: but no man laid hands on him, because his hour was not yet come.
Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
31 But many of the multitude believed on him, and said, When the Messiah cometh, will he do greater miracles than those which this man doth?
Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
32 The Pharisees heard the people muttering these things respecting him; and the Pharisees and chief priests sent officers to apprehend him.
Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
33 Then said Jesus unto them, A little while longer I am with you, and I am going to him that sent me.
Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
34 Ye shall seek me, and shall not find me: and where I am, ye cannot come.
Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
35 Then said the Jews among themselves, Whither will this man go, that we shall not find him? will he go to the dispersed among the Grecians, and teach the Greeks?
Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
36 What is this saying which he hath spoken, Ye shall seek me, and shall not find me: and where I am, ye cannot come?
Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
37 Now on the last day, the great day of the feast, Jesus stood up and spake aloud, saying, If any man thirst, let him come unto me and drink.
Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
38 He that believeth on me, as the scripture hath said, from his belly shall rivers flow of living water.
Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
39 (Now he spake this in reference to the Spirit, which they who believe on him should afterwards receive: for as yet the Holy Ghost was not given; because Jesus was not yet glorified.)
Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
40 Many then of the multitude, when they heard this declaration, said, This man is certainly a prophet.
Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
41 Others said, He is the Messiah. But others said, No: for cometh the Messiah out of Galilee?
Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
42 Doth not the scripture say, That the Messiah cometh of the seed of David, and from the town of Bethlehem, whence David originally was?
Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
43 There was a division therefore among the multitude on account of him.
Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
44 Now some of them were desirous to apprehend him; but no one laid hands upon him.
Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
45 Then came the officers to the chief priests and Pharisee; and they said to them, Why have ye not brought him?
Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
46 The officers answered, Never did man before speak in such a manner as this man.
Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
47 The Pharisees then replied to them, Are ye also deluded?
Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
48 Hath any one of the rulers or of the Pharisees believed on him?
Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
49 But this rabble, which knoweth not the law, is accursed.
Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
50 Nicodemus saith unto them, (the same person who came to him by night, being one of their body, )
Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
51 Doth our law condemn a man, without first hearing his defence, and knowing what he hath done?
“Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
52 They answered and said to him, Art thou not from Galilee too? Search and see: for a prophet, out of Galilee, never was raised up.
Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
53 So each went to his own home.
(Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.