< Mark 4 >

1 And again He began to teach by the sea: and a great multitude is gathered unto Him, so that He having gone into a ship, sat on the sea; and the whole multitude was at the sea on the land.
Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
2 And He was teaching them many things in parables, and in His teaching He said to them,
Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
3 Hear: Behold, a sower went out to sow:
“Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4 and it came to pass while he was sowing, some fell by the wayside, and the fowls came and devoured it.
Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5 And other fell upon stones, where it had not much earth; and immediately it sprang up, because it had no depth of earth:
Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6 and when the sun arose, it was scorched; and because it had no root, it withered away.
Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7 And other fell among thorns, and the thorns sprang up, and choked it, and it gave no fruit.
Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
8 And other fell in good ground, and springing up and growing, gave fruit, and produced, one thirty, and one sixty, and one a hundred.
Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.”
9 And He said, Let the one having ears to hear, hear.
Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
10 And when they were alone, and those around Him along with the twelve asked Him the parable.
Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
11 And He said to them, To you it has been given the mystery of the kingdom of God: but to them who are without, all things are in parables:
Naye akawaambia, “Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
12 in order that seeing they may see, and not know; and hearing they may hear, and not understand; lest they may turn, and their sins may he forgiven unto them.
ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.”
13 And He says to them, Do you not understand this parable? and how will you know all parables?
Basi, Yesu akawauliza, “Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
14 The sower sows the word.
Mpanzi hupanda neno la Mungu.
15 And those who are by the way-side, where the word is sown; and when they hear it, immediately Satan comes, and takes away the word which was sown in their hearts.
Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
16 And those who are sowed upon the rocks are likewise, those who, when they may hear the word, immediately with joy receive it.
Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
17 And they have no root in themselves, but are temporary; then tribulation or persecution arising on account of the word, they are immediately offended:
Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
18 and others are those who are sown among the thorns; they are those hearing the word,
Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
19 and the cares of the age, and the deceitfulness of riches, and desires concerning other things coming into them, choke out the word, and it becomes unfruitful. (aiōn g165)
lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn g165)
20 And these are they who are sown on good ground; whosoever hear the word, and receive it, and bring forth fruit, some thirty, some sixty, and some a hundred.
Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja.”
21 And He said to them; Whether does the light come, that it may be placed under a bushel, or under a bed? is it not that it may be placed on a candlestick?
Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
22 For there is nothing hidden which may not be made manifest; neither is there any thing concealed, but that it may come into the light.
Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
23 If any one has ears to hear, let him hear.
Mwenye masikio na asikie!”
24 And He said to them. See what you hear: with what measure you measure it shall be measured unto you: and it shall be added unto you who hear.
Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
25 For whosoever has, it shall be given unto him: and he who has not, it shall be taken from him even that which he has.
Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”
26 And He said, Thus is the kingdom of God, as a man may cast seed on the ground;
Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
27 and he may sleep, and rise night and day, and the seed germinates and grows, as he does not know.
Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
28 The earth spontaneously brings forth fruit; first the blade, then the ear, then the full corn in the ear.
Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
29 And when the fruit may develop, immediately he thrusts in the sickle, because the harvest is at hand.
Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
30 And He said, To what may we liken the kingdom of God? or in what parable may we present it?
Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
31 Tis like a grain of mustard seed, which when it may be sown upon the earth, is the smallest of all seeds which are upon the earth,
Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
32 and when it may be sowed, it springs up, and becomes the greatest of herbs, and produces great branches; so that the birds of the heavens are able to lodge under its shadow.
Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.”
33 And in many such parables He continued to speak the word to them, as they were able to hear.
Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
34 And without a parable He did not speak to them: and He privately expounded all things to His disciples.
Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
35 And He says to them, on that day, it being evening, Let us go away to the other side.
Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ng'ambo.”
36 And leaving the multitude, they receive Him, as He was in the ship; and other ships were also with Him.
Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
37 And there was a great storm of wind: and the waves were dashing into the ship, so that it was already filled.
Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
38 And He was in the stern, sleeping on a pillow: and they awaken Him, and say to Him; Teacher, is there no care to thee that we perish?
Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?”
39 And being awakened, He said to the sea, Be calm, be quiet. And the wind ceased, and there was a great calm.
Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
40 And He said to them, Why are you so cowardly? how have you not faith?
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?”
41 And they feared with a great fear, and continued to say to one another, Who then is this, because the wind and the sea obey Him?
Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< Mark 4 >