< Mark 15 >
1 And immediately early in the morning the high priests having made counsel with the elders and scribes, and all the sanhedrim, having bound Jesus, led Him away, and delivered Him to Pilate.
Kulipopambazuka, makuhani wakuu walifanya shauri pamoja na wazee, walimu wa Sheria na Baraza lote, wakamfunga Yesu pingu, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato.
2 And Pilate asked Him, Art thou the King of the Jews? And responding He says to him, Thou sayest it.
Pilato akamwuliza Yesu, “Je, wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu akajibu, “Wewe umesema.”
3 And the chief priests were accusing Him of many things.
Makuhani wakuu wakamshtaki Yesu mambo mengi.
4 And Pilate again asked Him, saying, Do you not answer? behold, how many things they witness against you.
Pilato akamwuliza tena Yesu, “Je, hujibu neno? Tazama wanavyotoa mashtaka mengi juu yako.”
5 And Jesus responded nothing at all; so that Pilate marveled.
Lakini Yesu hakujibu neno, hata pilato akashangaa.
6 But during the feast he was accustomed to release unto them one prisoner, whom they asked,
Kila wakati wa sikukuu ya Pasaka, Pilato alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa mmoja waliyemtaka.
7 And there was one called Barabbas, having been bound along with the insurrectionists, who had committed murder during the insurrection.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Baraba, ambaye alikuwa amefungwa pamoja na waasi wengine kwa kusababisha uasi na mauaji.
8 And the multitude crying out began to ask, as he was always accustomed to do unto them.
Watu wengi wakamwendea Pilato wakamwomba awafanyie kama kawaida yake.
9 And Pilate responded to them, saying, Do you wish that I may release unto you the King of the Jews?
Pilato akawauliza, “Je, mwataka niwafungulieni Mfalme wa Wayahudi?”
10 For he knew that the chief priests had delivered Him on account of envy.
Alisema hivyo kwa sababu alijua wazi kwamba makuhani wakuu walimkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.
11 And the chief priests persuaded the multitude that he should rather release unto them Barabbas.
Lakini makuhani wakuu wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba.
12 And Pilate responding again said to them, Then what do you wish that I shall do unto Him whom you call the King of the Jews.
Pilato akawauliza tena, “Basi, sasa mwataka nifanye nini na mtu huyu mnayemwita Mfalme wa Wayahudi?”
13 And they again cried out, Crucify Him.
Watu wote wakapaaza sauti tena: “Msulubishe!”
14 And Pilate said to them, For what evil hath He done? And they cried out uproariously, Crucify Him.
Lakini Pilato akawauliza, “Kwa nini! Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupaaza sauti, “Msulubishe!”
15 And Pilate, wishing to do the multitude a favor, released unto them Barabbas. And having scourged Jesus, he delivered Him up that He should be crucified.
Pilato alitaka kuuridhisha huo umati wa watu; basi, akamwachilia Baraba kutoka gerezani. Akaamuru Yesu apigwe viboko, kisha akamtoa asulubiwe.
16 And the soldiers led Him into the court, which is the judgment hall; and call around Him the whole band.
Kisha askari walimpeleka Yesu ndani ukumbini, katika ikulu, wakakusanya kikosi kizima cha askari.
17 And they put on Him a purple robe, and having plaited a thorny crown, put it on Him.
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamwekea kichwani.
18 And they began to mock Him, Hail, King of the Jews!
Wakaanza kumsalimu, “Shikamoo Mfalme wa Wayahudi!”
19 And they continued to strike His head with a reed, and spit on Him, and putting down their knees worshiped Him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi, wakamtemea mate; wakampigia magoti na kumsujudia.
20 And when they mocked Him, they divested Him of the purple robe, and put on Him His own raiment: and lead Him away in order that they may crucify Him.
Baada ya kumdhihaki, walimvua lile joho, wakamvika nguo zake, kisha wakampeleka kumsulubisha.
21 And they compel a certain Simon, a Cyrenean, coming from the country, the father of Alexander and Rufus, that he must take His cross.
Walipokuwa njiani, walikutana na mtu mmoja aitwaye Simoni, mwenyeji wa Kurene. Yeye alikuwa baba wa Aleksanda na Rufo, na wakati huo alikuwa akitoka shambani. Basi, wakamlazimisha auchukue msalaba wa Yesu.
22 And they lead Him to Golgotha, a place which is interpreted, The place of a skull.
Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, “Mahali pa Fuvu la Kichwa.”
23 And they gave Him myrrhed wine to drink: and He did not take it.
Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye akaikataa.
24 And they crucify Him, and divide His garments, casting the lot upon them, what each one may take.
Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.
25 And it was the third hour, and they crucified Him.
Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.
26 And the superscription of His accusation was written over Him, THE KING OF THE JEWS.
Na mshtaka wake ulikuwa umeandikwa: “Mfalme wa Wayahudi.”
27 And they crucify two thieves along with Him; the one on His right, and one on His left.
Pamoja naye waliwasulubisha wanyang'anyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”
29 And passing by they continued to blaspheme Him, wagging their heads, and saying, Aha, thou that destroyest the temple, and buildest it in three days,
Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu!
30 save thyself, and come down from the cross.
Sasa, shuka msalabani ujiokoe mwenyewe!”
31 Likewise also the chief priests mocking to one another with the scribes, continued to say, He saved others; He is not able to save Himself.
Nao makuhani wakuu pamoja na walimu wa Sheria walimdhihaki wakisema, “Aliwaokoa wengine, lakini kujiokoa mwenyewe hawezi!
32 Let Christ, the King of Israel, now come down from the cross, in order that we may see and believe. And those being crucified along with Him were reproaching Him.
Eti yeye ni Kristo, Mfalme wa Israeli! Basi, na ashuke msalabani ili tuone na kuamini.” Hata watu wale waliosulubiwa pamoja naye walimtukana.
33 And it being the sixth hour, there was darkness over all the earth until the ninth hour.
Tangu saa sita mchana mpaka saa tisa kulikuwa giza nchini kote.
34 And at the ninth hour Jesus cried with a loud voice, saying, Eloi, Eloi, lama sabachthani? which is interpreted, My God, my God, why hast thou forsaken me?
Saa tisa alasiri Yesu akalia kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lema sabakthani?” Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
35 And certain ones of those standing by said, Behold, He is calling Elijah.
Baadhi ya watu waliosimama pale waliposikia hivyo, walisema, “Sikiliza! Anamwita Eliya!”
36 And one running and filling a sponge with vinegar, and reaching it forth on a reed, gave Him drink, saying, Let Him alone, let us see if Elijah comes to take Him down.
Mtu mmoja akakimbia, akachovya sifongo katika siki, akaiweka juu ya mwanzi, akampa anywe akisema, “Hebu tuone kama Eliya atakuja kumteremsha msalabani!”
37 And Jesus, sending forth a loud voice, expired.
Yesu akapaaza sauti kubwa, akakata roho.
38 And the veil of the temple was rent in twain from top even to the bottom.
Basi, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 And the centurion standing by in front of Him, seeing that He thus expired, said; Surely this man was the Son of God.
Jemadari mmoja aliyekuwa amesimama mbele yake aliona jinsi Yesu alivyolia kwa sauti na kukata roho, akasema, “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40 And there were women looking on from a distance: among whom was Mary Magdalene, and Mary the mother of James the less and Joses, and Salome;
Walikuwako pia wanawake waliotazama kwa mbali, miongoni mwao akiwa Maria toka mji wa Magdala, Salome, na Maria mama wa kina Yakobo mdogo na Yose.
41 who when He was in Galilee, were accustomed both to follow Him, and minister unto Him. And many other women who came up to Jerusalem along with Him.
Hawa walimfuata Yesu alipokuwa Galilaya na kumtumikia. Kulikuwa na wanawake wengine wengi waliokuja Yerusalemu pamoja naye.
42 And it already being evening, since it was the Preparation, which is the day before the Sabbath,
Wakati wa jioni ulikuwa umekwisha fika. Hiyo ilikuwa siku ya Maandalio, yaani siku inayotangulia Sabato.
43 Joseph, who is from Arimathea, an honorable councilor, who also himself was waiting for the kingdom of God; having taken courage came to Pilate, and begged the body of Jesus.
Hapo akaja Yosefu mwenyeji wa Armathaya, mjumbe wa Baraza Kuu, aliyeheshimika sana. Yeye pia alikuwa anatazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Basi, alimwendea Pilato bila uoga, akaomba apewe mwili wa Yesu.
44 And Pilate was astonished if He had died already. And having called the centurion, asked him if He was already dead.
Pilato alishangaa kusikia kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa. Basi, akamwita jemadari, akamwuliza kama Yesu alikuwa amekufa kitambo.
45 And having learned from the centurion, he gave the body to Joseph.
Pilato alipoarifiwa na huyo jemadari kwamba Yesu alikuwa amekwisha kufa, akamruhusu Yosefu auchukue mwili wake.
46 And having purchased linen, and taking Him down, he wrapped Him in the linen, and placed Him in a sepulcher which had been hewn out of the rock; and he rolled a stone to the door of the sepulcher.
Hapo Yosefu akanunua sanda ya kitani, akauteremsha chini huo mwili, akauzungushia sanda. Akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa mwambani, kisha akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango.
47 And Mary Magdalene and Mary the mother of Joses were looking where He is placed.
Nao Maria Magdalene na Maria mama yake Yose walipaona hapo alipolazwa.