< Luke 2 >

1 It came to pass in those days, a decree went out from Augustus Caesar, to enroll all the world.
Sasa katika siku hizo, ikatokea kwamba Kaisari Agusto alitoa agizo akielekeza kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi duniani.
2 This was the first enrollment, Cyrenius being governor of Syria.
Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio akiwa gavana wa Siria.
3 And all were going forth to enroll, each one into his own city.
Hivyo kila mmoja akaenda mjini kwake kuandikishwa sensa.
4 And Joseph also went up from Galilee, out of the city Nazareth, into Judea, into the city of David which is called Bethlehem, because he was of the house and family of David,
Naye Yusufu aliondoka pia katika mji wa Nazareti huko Galilaya na akasafiri Yudea katika mji wa Bethlehemu, ujulikanao kama mji wa Daudi, kwa sababu alitokea katika ukoo ya Daudi.
5 to enroll himself along with Mary, the wife having been betrothed to him, being in an advanced state of pregnancy.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Mariamu, ambaye alikuwa amemposa na alikuwa akitazamia mtoto.
6 And it came to pass while they were there the days of her parturition were fulfilled.
Sasa ilitokea kwamba, wakiwa kule wakati wake wa kujifungua mtoto ukawadia.
7 And she brought forth her firstborn son, and she wrapped Him in swaddling clothes and laid Him in a manger, because there was no place for them in the inn.
Akajifungua mtoto wa kiume, mzaliwa wake wa kwanza, akamzungushia nguo mwilini kumkinga na baridi mtoto. Ndipo akamweka kwenye kihori cha kulishia wanyama, kwa sababu haikuwepo nafasi kwenye nyumba za wageni.
8 And the shepherds were in that country, tenting out and keeping guard over their flock by night.
Katika eneo hilo, walikuwapo wachungaji walioishi mashambani wakilinda makundi ya Kondoo wao usiku.
9 And behold an angel of the Lord stood over them and the glory of the Lord shone around them; and they feared with great fear.
Ghafla, malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukang'aa kuwazunguka, na wakawa na hofu sana.
10 And the angel said to them; Fear not; for behold, I preach unto you the gospel of great joy, which shall be to all people;
Ndipo malaika akwaambia, “Msiogope, kwasababu nawaletea habari njema ambayo italeta furaha kuu kwa watu wote.
11 because this day a Savior is born unto you, who is Christ the Lord, in the city of David.
Leo Mwokozi kazaliwa kwaajili yenu mjini mwa Daudi! Yeye ndiye Kristo Bwana!
12 And this shall be the sign unto you; you shall find an infant lying in a manger, wrapped in swaddling clothes.
Hii ndiyo ishara ambayo mtapewa, mtamkuta mtoto amefungwa nguo na amelala kwenye hori la kulishia wanyama.”
13 And immediately a multitude of the heavenly host was with the angel, praising God and saying;
Ghafla kukawa na jeshi kubwa la mbinguni likaungana na malaika huyo wakamsifu Mungu, wakisema,
14 Glory to God in the highest, and peace on earth; good will among men.
“Utukufu kwa Mungu aliye juu sana, na amani iwe duniani kwa wote ambao anapendezwa nao.”
15 And it came to pass, when the angels departed from them into heaven, indeed, the shepherds said to one another; Now let us go unto Bethlehem and see this word which has taken place, which the Lord made known to us.
Ikawa kwamba malaika walipokwisha kuondoka kwenda mbinguni, wachungaji wakasemezena wao kwa wao, “Twendeni sasa kule Bethlehemu, na tukaone hiki kitu ambacho kimetokea, ambacho Bwana ametufahamisha.”
16 They went making haste, and found both Mary and Joseph, and the infant lying in the manger.
Wakaharakisha kule, na wakamkuta Mariamu na Yusufu, na wakamuona mtoto amelala kwenye hori la kulishia wanyama.
17 And seeing, they made known concerning the word which was spoken to them about this little child.
Na walipoona hivi, wakawajulisha watu kile walichokuwa wameambiwa kumhusu mtoto.
18 And all hearing wondered concerning the things which were spoken to them by the shepherds.
Wote waliosikia habari hii wakashangazwa na kile kilichosemwa na wachungaji.
19 And Mary kept all these words laying them up in her heart.
Lakini Mariamu akaendelea kufikiri kuhusu yote aliyokwisha kuyasikia, akiyatunza moyoni mwake.
20 And the shepherds returned, glorifying and praising God, for all things which they heard and saw, as it was spoken to them.
Wachungaji wakarudi wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya kila kitu walichokwisha sikia na kuona, kama tu ilivyokuwa imenenwa kwao.
21 And when the eight days of circumcising Him were fulfilled, and His name was called Jesus, having been called by the angel before He was conceived in the womb.
Ilipofika siku ya nane na ilikuwa ni wakati wa kumtahiri mtoto, wakamwita jina Yesu, jina alilokwishapewa na yule malaika kabla mimba haijatungwa tumboni.
22 And when the days of their purification were fulfilled, according to the law of Moses, they carried him up into Jerusalem, to present him to the Lord,
zao zilizotakiwa za utakaso zilipopita, kulingana na sheria ya Musa, Yusufu na Mariamu wakampeleka hekaluni kule Yerusalemu kumweka mbele za Bwana.
23 as it was written in the law of the Lord; That every male opening the womb shall be called holy to the Lord;
Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, “Kila mwanaume anayefungua tumbo ataitwa aliyetolewa wakfu kwa Bwana.”
24 and to offer a sacrifice according to that which has been written in the law of the Lord, a pair of turtle-doves, or two young pigeons.
Wao vilevile walikuja kutoa sadaka kulingana na kile kinachosemwa katika sheria ya Bwana, “Jozi ya njiwa au makinda mawili ya njiwa.”
25 And behold, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon; and the same man was righteous and godly, awaiting the consolation of Israel, and the Holy Spirit was on him;
Tazama, palikuwa na mtu katika Yerusalemu ambaye jina lake alikuwa akiitwa Simeoni. mtu huyu alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Yeye alikuwa akisubiri kwa ajili ya mfariji wa Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 and it was revealed unto him by the Holy Spirit, that he should not see death before he may see the Christ of the Lord.
Ilikuwa imekwisha funuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu kwamba yeye hangelikufa kabla ya kuwomwona Kristo wa Bwana.
27 And he came in the Spirit into the temple; and while the parents are bringing in the little child Jesus, that they may do according to the provisions of law concerning Him,
Siku moja alikuja ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho Mtakatifu. Ambapo wazazi walimleta mtoto, Yesu, kumfanyia yale yaliyopasa kawaida ya sheria,
28 he received Him into his arms and blessed God and said;
ndipo Simeoni alimpokea mikononi mwake, na akamsifu Mungu na kusema,
29 Now, O Lord, thou art letting thy servant depart, in peace according to thy word;
“Sasa ruhusu mtumishi wako aende kwa amani Bwana, kulingana na Neno lako.
30 because mine eyes saw thy salvation,
Kwa kuwa macho yangu yameuona wakovu wako,
31 which thou didst prepare before the face of all peoples;
ambao umeonekana kwa macho ya watu wote.
32 a light unto the revelation of the Gentiles, and the glory of thy people Israel.
Yeye ni nuru kwa ajili ya ufunuo kwa Wamataifa na utukufu wa watu Israeli.”
33 And His father and His mother were marveling at the words spoken concerning Him.
Baba na Mama wa mtoto walishangazwa kwa mambo ambayo yalizungumzwa juu yake.
34 And Simeon blessed them and said to Mary, His mother; Behold, he is appointed unto the fall and rising of many in Israel, and unto a sign which is spoken against;
Ndipo Simeoni akawabariki na akasema kwa Mariamu mama yake, “Sikiliza kwa makini! Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli na ni ishara ambayo watu wengi wataipinga.
35 and a sword shall go through thy soul, in order that the reasonings of many hearts may be revealed.
Pia ni upanga utakaochoma nafsi yako mwenyewe, ili kwamba mawazo ya mioyo ya wengi yadhihirike”.
36 And Anna was a prophetess, the daughter of Phanuel of the tribe of Asher, herself being advanced in many days, having lived with her husband seven years from her virginity;
Nabii mwanamke aliyeitwa Ana pia alikuwako hekaluni. Yeye alikuwa binti wa Fanueli kutoka kabila la Asheri. Alikuwa na miaka mingi sana. Naye aliishi na mume wake kwa miaka saba baada ya kuoana,
37 and she a widow of about fourscore years, who did not depart from the temple, worshiping night and day with fastings and prayers.
na ndipo akawa mjane kwa miaka themanini na minne. Naye hakuwahi kuondoka hekaluni na alikuwa akiendelea kumwabudu Mungu pamoja na kufunga na kuomba, usiku na mchana.
38 And she, at the same hour, standing up continued to praise the Lord, and speak concerning Him to all those awaiting the redemption in Jerusalem.
Na kwa wakati huo, alikuja pale walipo akaanza kumshukuru Mungu. Aliongea kumhusu mtoto kwa kila mtu ambaye alikuwa akisubiri ukombozi wa Yerusalemu.
39 And when they finished all things according to the law of the Lord, they returned into Galilee into their own city Nazareth.
Walipomaliza kila kitu walichotakiwa kufanya kuligana na na sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, mjini kwao, Nazareti.
40 And the child continued to grow and waxed strong in spirit, being full of wisdom; and the grace of God was on Him.
Mtoto alikua, na akawa na nguvu, akiongezeka katika hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 And His parents were going, according to custom, into Jerusalem at the feast of the passover.
Wazazi wake kila mwaka walikwenda Yerusalemu kwaajili ya sikukuu ya Pasaka.
42 And when He was twelve years old, they going up to Jerusalem according to the custom of the feast,
Alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walikwenda tena wakati mwafaka kidesturi kwa ajili ya sikukuu.
43 and having completed the days, while they were returning the boy Jesus remained in Jerusalem. And His parents knew it not.
Baada ya kubaki siku zote kwa ajili ya sikukuu, walianza kurudi nyumbani. Lakini mvulana Yesu alibaki nyuma mle Yerusalemu na wazazi wake hawakujua hili.
44 And thinking that He is in the crowd, they came a day's journey, and were seeking Him among His relatives and acquaintances.
Walidhani kwamba yumo kwenye kundi walilokuwa wakisafiri nalo, hivyo walisafiri safari ya siku. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni wa ndugu na marafiki zao.
45 And not having found Him; they returned to Jerusalem seeking Him.
Waliposhindwa kumpata, walirudi Yerusalemu na wakaanza kumtafuta humo.
46 And it came to pass, after three days they found Him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both hearing them and asking them questions.
Ikatokea kwamba baada ya siku tatu, wakampata hekaluni, akiwa ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 And all hearing Him were astonished at His wisdom and answers.
Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
48 And seeing Him they were astonished, and His mother said to Him; Child, why did you thus do unto us? Behold, thy father and I were seeking thee, sorrowful.
Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
49 And He said to them, Why were you seeking after me? Did you not know that it behooved me to be in the affairs of my Father?
Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
50 And they did not understand the word which He spoke unto them.
Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
51 And He went down with them and came to Nazareth; and was subject unto them. And His mother continued to keep all these words in her heart.
Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
52 And Jesus continued to grow in wisdom and stature and favor with God and men.
Lakini Yesu aliendelea kukua katika hekima na kimo, na akazidi kupendwa na Mungu na watu.

< Luke 2 >