< Jude 1 >

1 Jude, the servant of Jesus Christ, and brother of James, to the called beloved in God the Father, and kept in Jesus Christ.
Yuda, mtumwa wa Yesu Kristo, na ndugu yake Yakobo, kwa wale ambao wameitwa, wapendwao katika Mungu Baba, na waliotunzwa kwa ajili ya Yesu Kristo:
2 Mercy to you, and peace, and divine love be multiplied.
rehema na amani na upendo viongezwe kwenu.
3 Beloved, making all haste to write to you concerning our common salvation, I had need to write to you, exhorting you to agonize for the faith which was once delivered unto the saints.
Wapenzi, wakati nilipokuwa nikifanya kila juhudi kuwaandikia ninyi kuhusu wokovu wetu sote, ilinilazimu kuwaandikia kwa ajili ya kuwashauri ili mshindanie kwa uaminifu imani ambayo ilikuwa imekabidhiwa mara moja tu kwa waamini.
4 For certain men have crept in, who long ago were written down to this judgment, ungodly, transforming the grace of God into impurity, even denying Jesus Christ, our only Sovereign and Lord.
Kwa sababu watu fulani wamejiingiza kwa siri kati yenu - watu ambao walitiwa alama kwa ajili ya hukumu - watu wasio wataua ambao hubadili neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, na kumkana Bwana wetu pekee na Bwana Yesu Kristo.
5 But I wish you to remember, once having known all these things, that the Lord, having saved the people out of the land of Egypt, destroyed them that believed riot, the second time:
Sasa napenda kuwakumbusha ninyi ingawa kuna wakati mlijua kwa ukamilifu kwamba Bwana aliwaokoa watu kutoka nchi ya Misri, lakini baadaye kuwaangamiza wale ambao hawakuamini.
6 and the angels who kept not their first estate, but left their own habitation, has he kept in eternal chains unto darkness unto the judgment of the great day: (aïdios g126)
Na malaika ambao hawakuilinda enzi yao wenyewe lakini wakaacha makao yao maalum Mungu amewaweka katika minyororo ya milele, ndani ya giza, kwa ajili ya hukumu ya siku ile kuu. (aïdios g126)
7 as Sodom and Gomorrah and the cities about them, in a manner like unto them committing fornication, and going after other flesh, present an example receiving the vengeance of eternal fire. (aiōnios g166)
Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyoizunguka, ambayo pia ilijiingiza yenyewe katika uasherati na wakafuata tamaa isiyo ya asili. Walioneshwa kama mifano ya wale ambao huteseka katika hukumu ya moto wa milele. (aiōnios g166)
8 Likewise indeed these dreamers also pollute the flesh, and reject lordship, and blaspheme glories.
Hali kadhalika, kwa njia ile ile waota ndoto hawa pia huchafua miili yao, na hukataa mamlaka, na wananena uongo dhidi ya mtukufu.
9 But Michael the archangel, when contending with the devil he disputed over the body of Moses, did not dare to bring against him a judgment of blasphemy, but said, The Lord rebuke thee.
Lakini hata Mikaeli malaika mkuu, wakati alipokuwa akishindana na ibilisi na kuhojiana naye kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kuleta hukumu ya uongo dhidi yake, lakini badala yake alisema, “Bwana akukemee!”
10 But these blaspheme so many things as they know not: and so many things as they understand naturally, like irrational animals, in these they are corrupted.
Lakini watu hawa huleta uongo dhidi ya chochote wasicho kifahamu. Na kile wasicho kifahamu- kile ambacho wanyama wasio na akili hujua kwa silika- haya ndiyo yaliyo waharibu.
11 Woe unto them! because they have gone off in the way of Cain, and in the delusion of Balaam they have been seduced by reward, and they perished in the gainsaying of Korah.
Ole wao! Kwa kuwa wametembea katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu. Wameangamia katika uasi wa Kora.
12 These are rocks in your love-feasts, feasting along with you without fear shepherdizing themselves, clouds without water, driven away by the winds; withered trees, without fruit, twice dead, plucked up by the roots;
Hawa ni miamba katika sherehe zenu za upendo, wakisherehekea bila aibu, wakijilisha tu wenyewe. Ni mawingu yasiyo na maji, yanayobebwa na upepo, ni miti iliyopukutika isiyo na matunda iliyo kufa mara mbili, iliyong'olewa mizizi
13 wild waves of the sea, foaming out their own disgraces; wandering stars, for which the blackness of darkness has been reserved forever. (aiōn g165)
Ni mawimbi ya bahari yenye kelele yakitoa aibu yao wenyewe, Ni nyota zinazorandaranda ambazo weusi wa giza umetunzwa kwa ajili yao milele. (aiōn g165)
14 And Enoch also, the seventh from Adam, prophesied against these, saying, Behold, the Lord came with his myriads of saints,
Enoko, wa saba katika orodha ya Adamu, alitabiri kuhusu wao, akisema, “Tazama! Bwana anakuja na maelfu kwa maelfu ya watakatifu wake,
15 to execute judgment against all, and to convict all the ungodly of them for all the works of their ungodliness which they have impiously done, and for all their hard speeches which they have spoken against him, being ungodly sinners.
ili afanye hukumu juu ya kila mtu, na kutia hatia wote wasiomcha Mungu juu ya matendo yao yote waliyokwishafanya katika njia zisizo za kitauwa, na kwa maneno yote ya ukali ambayo wasio watauwa wameyanena dhidi yake.”
16 These are querulous grumblers, going forth according to their own lusts; and their mouth speaking swelling words, admiring persons for the sake of gain.
Hawa ni wale wanung'unikao, walalamikao ambao hufuata tamaa zao za uovu, wajivunao mno, ambao kwa faida yao hudanganya wengine.
17 But you, beloved, remember the words which have hitherto been spoken by the apostles of our Lord Jesus Christ;
Lakini ninyi, wapenzi, kumbukeni maneno ambayo yalinenwa zamani na mitume wa Bwana Yesu Kristo.
18 that they said to you, At the last time there will be mockers, walking according to their own lusts after ungodly things.
Walisema kwenu, “Katika wakati wa mwisho kutakuwa na watu wanaodhihaki ambao hufuata tamaa zao zisizo za kitauwa.”
19 These are they who are sidetracking [the people], intellectual, not having the Spirit.
Watu hawa ni watenganishaji, wanatawaliwa na tamaa za asili, na hawana Roho.
20 But you, beloved, building up yourselves on your most holy faith, praying in the Holy Ghost,
Lakini ninyi, wapenzi, kama mjijengavyo katika imani yenu takatifu sana, na kama muombavyo katika Roho Mtakatifu,
21 keep yourselves in the divine love of God, receiving the mercy of our Lord Jesus Christ unto eternal life. (aiōnios g166)
jitunzeni katika upendo wa Mungu, na msubiri rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo ambayo huwapatia uzima wa milele. (aiōnios g166)
22 And some of whom indeed convict, being judged:
Onesheni rehema kwa wale walio na shaka.
23 and some save, seizing them out of the fire; and some pity in their fear, you indeed hating the garment having been spotted by carnality.
Waokoeni wengine kwa kuwanyakua kutoka katika moto. Kwa wengine onesheni huruma kwa hofu, mkichukia hata vazi lililotiwa doa na mwili.
24 But to him who is able to keep you from falling, and to establish you blameless in the presence of his glory with rejoicing.
Sasa kwake awezaye kuwalinda msijikwae, na kuwasababisha msimame mbele ya utukufu wake, bila mawaa na kuwa na furaha kuu,
25 to God our only Saviour, through Jesus Christ our Lord, be glory, majesty, dominion and power, before every age, both now, and unto all the ages. Amen. (aiōn g165)
kwake Mungu pekee mwokozi kupitia Yesu Kristo Bwana wetu, utukufu uwe kwake, ukuu, uwezo na nguvu kabla ya nyakati zote, na sasa na hata milele. Amina. (aiōn g165)

< Jude 1 >