< John 21 >

1 After these things, Jesus again manifested Himself to His disciples, at the Sea of Tiberias; and He thus manifested Himself.
Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
2 Simon Peter, and Thomas called Didymus, and Nathanael the one from Cana of Galilee, and the sons of Zebedee, and two others of His disciples, were together.
Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
3 Simon Peter says to them, I go to fish. They say to Him, We also go along with you. They went out, and entered into a ship, and that night caught nothing.
Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
4 And it being now morning, Jesus stood on the shore: the disciples did not know that He is Jesus.
Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
5 Then Jesus says to them; Little children, whether have you any meat? They respond to Him, No.
Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
6 He says to them, Cast the net to the right side of the ship, and you will find: then they cast it, and were not able to draw it on account of the multitude of the fishes.
Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
7 Then that disciple whom Jesus loved said to Peter, He is the Lord. Then Simon Peter hearing that He is the Lord, girded on his fishing-cloak (for he was unclothed), and cast Himself into the sea:
Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
8 and the other disciples came in the ship (for they were not far from the land, but about two hundred cubits), drawing the net of the fishes.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
9 Then when they came to the land, they see fire lying, and fish and bread lying on it.
Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
10 Jesus said to them, Take from the fishes which you now caught.
Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
11 And Simon Peter came up, and drew the net to the land, full of a hundred and fifty-three large fishes: and there being so many yet the net was not broken.
Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
12 Jesus says to them, Come, take breakfast. But no one of the disciples dared to ask Him, Who art thou? knowing that He is the Lord.
Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
13 Jesus comes, and takes bread, and gives it to them, and fish likewise.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
14 And this third time Jesus was already manifested to His disciples, having risen from the dead.
Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
15 Then when they took breakfast, Jesus says to Simon Peter; Simon, the son of Jonah, dost thou love me with divine love more than these? He says to Him, Yes, Lord; thou knowest that I love thee as a friend. He says to him; Feed my lambs.
Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
16 Again He says to him a second time, Simon, the son of Jonah, do you love me with divine love? He says to Him; Thou knowest that I love thee as a friend. He says to him; Shepherdize my sheeplings.
Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
17 He says to him a third time; Simon, the son of Jonah, do you love me as a friend? Peter was grieved, because He said to him the third time, Do you love me as a friend? And he says to Him, Lord, thou knowest all things; and thou dost understand that I love thee as a friend. He says to Him, Feed my sheeplings.
Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
18 Truly, truly, I say unto you, When you were young, you girded yourself, and walked about where you wished: but when you get old, you will reach forth your hands, and another will lead you, where you do not wish.
Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
19 And He spoke this, signifying by what death he shall glorify God. And having spoken this, He says to him, Follow me.
Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
20 And Peter turning sees the disciple, whom Jesus loved, following; who also leaned upon His breast in the supper, and said; Lord, who is the one having betrayed thee?
Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
21 Then Peter seeing him says to Jesus; Lord, but what shall he do?
Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
22 And Jesus says to him, If I wish him to tarry until I come, what is that to thee?
Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
23 Then that word went out to the brethren that that disciple does not die. And Jesus did not say to him, that he does not die; but, If I wish him to tarry until I come.
Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
24 This is the disciple witnessing concerning these things, and having written the same: and we know that his testimony is true.
Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.

< John 21 >