< John 16 >
1 I have spoken these things to you, that you may not be offended.
Nimewaambia mambo haya ili msiweze kukwazwa.
2 They will put you out of the synagogues: but the hour is coming, that every one killing you may think he is offering service to God.
Watawatoa nje ya masinagogi; hakika saa inakuja ambayo kila atakayewaua atafikiri kuwa anafanya kazi njema kwa ajili ya Mungu.
3 And they will do these things, because they did not know the Father, nor me.
Watawatendea mambo haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi.
4 But I have spoken these things to you, that when the hour may come, you may remember them, that I did say them to you. But I said not these things to you from the beginning, because I was with you.
Nimewaambia mambo haya ili kwamba wakati ukifika wa haya kutokea, mnaweza kuyakumbuka na jinsi nilivyowaambia muweze wao. Sikuwaambia kuhusu mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I go to Him that sent me; and no one of you asks me, Whither goest thou?
Japokuwa, sasa naenda kwa yule aliyenituma; lakini hakuna kati yenu anayeniuliza, “Unaenda wapi?”
6 But because I have spoken these things to you, sorrow has filled your heart.
Kwa sababu nimesema maneno haya kwenu, huzuni imejaa mioyoni mwenu.
7 But now I tell you the truth; it is profitable to you that I may go away. For if I go not away, the Comforter will not come to you; but if I may go, I will send Him to you.
Hata hivyo, nawaambia ukweli: ni vyema kwenu nikiondoka; kwa maana nisipoondoka, mfariji hatakuja kwen; lakini nikienda ntamtuma kwenu.
8 And having come, He will convict the world concerning sin, and concerning righteousness, and concerning judgment.
Akija, huyo mfariji ataubitisha ulimwengu kuhusiana na dhambi, kuhusiana na haki na kuhusiana na hukumu.
9 Concerning sin indeed, because they do not believe on me; and concerning righteousness;
Kuhusiana na dhambi, kwa sababu hawakuniamini mimi,
10 because I go to the Father, and you see me no more;
kuhusiana na haki, kwa sababu naenda kwa baba, na hamtaniona tena;
11 and concerning judgment, because the prince of this world has been condemned.
na kuhusiana na hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amehukumiwa.
12 I have many things to say to you, but you are not able to bear them now.
Ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamtayaelewa sasa.
13 But when He, the Spirit of truth, may come, He will guide you in all truth: for He will not speak from Himself; but so many things as He hears, He will speak: and will proclaim to you the things which are coming.
Lakini, yeye, Roho wa kweli, akija, atawaongoza katika kweli yote; kwa kuwa hataongea kwa ajili yake mwenyewe; lakini yoyote atakayoyasikia, atayasema mambo hayo; na atayadhihirisha kwenu mambo yatakayokuja.
14 He will glorify me: because He will receive from mine, and proclaim them unto you.
Yeye atanitukuza mimi, kwa sababu atayachukua mambo yangu na atayatangaza kwenu.
15 And all things whatsoever the Father has are mine: therefore I said, that He takes from mine, and will proclaim them to you.
Vitu vyote alivyonavyo Baba ni vyangu; kwa hiyo, nimesema kwamba Roho atachukua mambo yangu na atayadhihirisha kwenu.
16 A little while, and ye see me no more; again a little while, and ye shall see me.
Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi tena, mtaniona.”
17 Then some of His disciples were saying to one another, What is this which He speaks to us, A little while, and you see me no more; and again a little while, and ye shall see me? and that I go to the Father?
Baadhi ya wanafunzi wake wakaambizana, “Ni nini anachotuambia, “muda mfupi, na hamtaniona tena,' na, kisha, mda mfupi mtaniona,' na, 'kwa sababu naenda kwa Baba?”
18 Then they were speaking, What is this, Little while, of which He speaks? and we know not what He is talking about.
Kwa hiyo wakasema, “Ni kitu gani anachosema, 'Bado mda mfupi'? Hatujui asemavyo.”
19 Jesus knew that they wished to ask Him, and said to them, You are seeking with one another concerning this, because I said, A little while, and you see me no more, and again a little while, and you shall see me?
Yesu aliona kuwa walitamani kumuuliza, naye akawaambia, “Mnajiuliza wenyewe kuhusu hili, nilivyosema, 'Bado muda mfupi, hamtaniona tena; na baada ya muda mfupi mtaniona'?
20 Truly, truly, I say unto you, that you will weep and mourn, and the world will rejoice; you will be sorrowful, but your sorrow will be turned into joy.
Amin, amin, nawaambia, mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utashangilia, mtakuwa na huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 When a woman may bring forth she has sorrow, because her hour has come: but when the little child may be born, she remembers her suffering no more, for the joy that a man has been born into the world.
Mwanamke anakuwa na huzuni wakati anapokuwa na uchungu kwa sababu wakati wa kujifungua umefika; lakini anapojifungua mtoto, hakumbuki tena maumivu kwa sababu ya furaha yake kwamba mtoto amezaliwa duniani.
22 Therefore you indeed also now have sorrow: but I will see you again, and your heart will rejoice, and no one taketh your joy from you.
Ninyi pia mna huzuni sasa, lakini nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi na hakuna atakayeweza kuiondoa furaha yenu.
23 And in that day you will ask of me nothing. Truly, truly, I say unto you, Whatsoever you may ask the Father, He will give it to you in my name.
Siku hiyo hamtaniuliza maswali. Amin, Amin, nawaambia, Mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu.
24 Until now you have asked nothing in my name: ask, and you shall receive, in order that your joy may be full.
Mpaka sasa hamjaomba lolote kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapokea ili kwamba furaha yenu ikamilike.
25 I have spoken these things unto you in parables; the hour comes, when I shall no longer speak to you in parables, but openly will I proclaim to you concerning the Father.
Nimezungumza na ninyi kwa lugha isiyoeleweka, lakini saa inakuja ambapo sitazungumza kwa lugha isiyoeleweka lakini badala yake nitawaambia waziwazi kuhusu Baba.
26 In that clay you shall ask in my name: and I do not say, that I will ask the Father for you;
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitaomba kwa Baba kwa ajili yenu;
27 for the Father Himself loves you, because you have loved me as a friend, and you have believed that I came out from God.
Kwa kuwa Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na kwa sababu mmeniamini kuwa nimetoka kwa Baba.
28 I came out from the Father, and have come into the world: again, I leave the world, and go to the Father.
Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni; tena, naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba”.
29 His disciples say; Behold, now you are talking openly, and speaking no parable.
Wanafunzi wake wakamwambia, “Unaona, sasa unaongea wazi wazi na hautumii mafumbo.
30 Now we know that you know all things, and have no need that any one may ask you: in this we believe that you came out from God.
Sasa, tunajua kwamba unajua mambo yote, na hauhitaji mtu yoyote akuulize maswali. Kwa sababu hii tunaamini kuwa unatoka kwa Mungu.
31 Jesus responded to them, Do you now believe?
Yesu akawajibu, “Sasa mmeamini?”
32 Behold, the hour cometh, and is already come, that you must be scattered abroad, each one to his own place, and leave me alone: I am not alone, because the Father is with me.
Tazama, saa inakuja, ndiyo na hakika imefika, ambapo mtatawanyika kila mmoja na kwa wa kwao mtaniacha mwenyewe. Lakini siko peke yangu kwa sababu Baba yupo nami.
33 I have spoken these things to you, in order that you may have peace in me. In the world you have tribulation: but take courage; I have conquered the world.
Nawaambia mambo haya ili kwamba ndani yangu muwe na amani. Duniani mna matatizo, lakini jipeni moyo, nimeushinda ulimwengu.