< Ephesians 1 >
1 Paul, the apostle of Jesus Christ through the will of God, to the saints who are in Ephesus, and to the faithful in Christ Jesus.
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Grace to you and peace from God our Father, and the Lord Jesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed is the God and Father of our Lord Jesus Christ, the one having blessed us with all spiritual blessing in the heavenlies in Christ:
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 as he elected us in himself before the foundation of the world, that we should be holy and blameless in his presence.
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 in love having predestinated us unto the adoption of sons unto himself through Jesus Christ, according to the good pleasure of his will,
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 unto the praise of the glory of his grace, with which he has blessed us in the Beloved:
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 in whom we have redemption through his blood, the remission of transgressions, according to the riches of his grace,
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 which he has abounded unto us in all wisdom and understanding,
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 having made known unto us the mystery of his will, according to his own good pleasure, which he purposed in himself
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 in the economy of the fulness of the times, to rehead all things in Christ, those in the heavens, and those upon the earth; in him,
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 in whom we were also chosen by lot, having been predestinated according to the purpose of him who works all things within us according to the counsel of his own will;
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 that we should be unto the praise of his glory, who first exercised hope in Christ:
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 in whom you also, having heard the word of truth, the gospel of your salvation, in whom, also having believed, you were sealed with the Holy Spirit of promise,
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 who is the earnest of our salvation, unto the redemption of the possession, unto the praise of his glory.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 Therefore I also, having heard of the faith among you in the Lord Jesus, and your love which is toward all the saints,
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 I do not cease giving thanks for you making mention of you in my prayers;
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 in order that the God of our Lord Jesus Christ, the Father of the glory, may grant unto you the spirit of wisdom and of revelation in the perfect knowledge of himself;
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 the eyes of your heart having been enlightened, that you may know what is the hope of his calling, what the riches of the glory of his inheritance among the saints,
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 and what the excellent majesty of his power toward us who believe, according to the working of the power of his might
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 which he has wrought in Christ, raising him from the dead, and seating him on his right hand in the heavenlies,
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 above all government, and authority, and power, and lordship, and every name named, not only in this age, but in the age to come: (aiōn )
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn )
22 and has subordinated all things beneath his feet, and given him to be head over all things to the church,
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 which is his body, the fulness of him who fills all things in all.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.