< Acts 26 >
1 And Agrippa said to Paul, It is permitted to thee to speak for thyself. Then Paul reaching forth his hand, proceeded with his defence:
Hivyo, Agripa akamwambia Paulo, `Unaruhusiwa kujitetea. ' Ndipo Paulo akanyoosha mkono wake akajitetea hivi.
2 O king Agrippa, I consider myself happy, being about this day to make my defence before thee concerning all those things of which I am accused by the Jews:
“Najiona mwenye furaha, Mfalme Agripa, ili kufanya kesi yangu mbele yako leo dhidi ya mashtaka yote ya Wayahudi.
3 especially as thou art acquainted with all the customs and questions among the Jews: therefore I pray you to hear me patiently.
Hasa, kwa sababu wewe ni mtaalamu wa desturi za Wayahudi na maswali. Hivyo naomba unisikilize kwa uvumilivu.
4 Moreover indeed all the Jews know my life from my youth; being from the beginning in my nation and in Jerusalem,
Kweli, Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu ujana wangu katika taifa langu huko Yerusalemu.
5 knowing me originally, if they may be willing to testify, that according to the most rigid sect of our religion I lived a Pharisee.
Wananijua tangu mwanzo na wanapaswa kukubali kwamba niliishi kama Mfarisayo, dhehebu lenye msimamo mkali kwenye dini yetu.
6 And now for the hope of the promise which is from God to our fathers, I stand being judged:
Sasa nimesimama hapa nihukumiwe kwa sababu mimi naliangalia ahadi ambayo Mungu aliifanya na baba zetu.
7 unto which our twelve tribes constantly worshiping night and day, hope to attain: concerning which hope I am accused by the Jews, O king.
Hii ni ahadi ambayo makabila yetu kumi na mbili yanatumaini kupokea kama wakimwabudu Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ni kwa ajili ya tumaini hili, mfalme Agripa, kwamba Wayahudi wananishitaki.
8 Why is it judged by you incredible, if God shall raise the dead?
Kwa nini yeyote kati yenu anafikiri ni ajabu kwamba Mungu hufufua wafu?
9 Moreover indeed, I thought to myself that I ought to do many things contrary to the name of Jesus the Nazarene:
Wakati mmoja nilifikiria mwenyewe kwamba ningefanya mambo mengi dhidi ya jina la Yesu wa Nazareti.
10 which I did also in Jerusalem, and shut up many of the saints in prison; and having received authority from the chief priests, and they being slain, I gave my vote against them;
Nilifanya haya katika Yerusalemu; Niliwafunga waamini wengi gerezani, na nilikuwa na mamlaka kutoka kwa wakuu wa makuhani kufanya hivyo; na wakati wanauawa, nilipiga kura dhidi yao.
11 and throughout all the synagogues, frequently punishing them, I compelled them to blaspheme; and being exceeding mad against them, I was persecuting them even also unto foreign cities.
Mara nyingi niliwaadhibu katika masinagogi yote na nilijaribu kuwafanya waikane imani yao. Nilikuwa na hasira sana juu yao na niliwafukuza hata katika miji ya ugenini.
12 Meanwhile journeying to Damascus with power and authority of the chief priests, I saw on the way, O king,
Wakati nilipokuwa nikifanya haya, nilienda Dameski, nikiwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa makuhani wakuu;
13 about midday, a light from heaven above the brightness of the sun, shining around me and those traveling with me;
nilipokuwa njiani wakati wa mchana, Mfalme, niliona mwanga kutoka mbinguni uliokuwa mkali kuliko jua na uling'aa kutuzunguka mimi na watu waliokuwa wakisafiri pamoja nami.
14 and we all having fallen to the ground, I heard a voice speaking to me in the Hebrew tongue, Saul, Saul, why persecutest thou me? it is hard for thee to kick against goads.
Sisi sote tulipoanguka chini, nalisikia sauti ikizungumza na mimi ikisema katika lugha ya Kiebrania: `Sauli, Sauli! Kwa nini unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.
15 And I said, Who art thou, Lord? And the Lord said, I am Jesus whom thou art persecuting.
Ndipo nikasema, 'Wewe ni nani, Bwana?' Bwana akajibu, 'Mimi ni Yesu ambaye unanitesa.
16 But rise up, and stand upon thy feet: for unto this have I appeared unto thee, to make thee a minister and a martyr both of those things which thou hast seen, and of which I will appear unto thee;
Sasa inuka usimame kwa miguu yako; sababu kwa kusudi hili mimi nimeonekana kwako, nimekuteua kuwa mtumishi na shahidi juu ya mambo ambayo unajua kuhusu mimi sasa na mambo nitakayokuonyesha baadaye;
17 delivering thee from the people, and from the Gentiles, unto whom now I send thee,
na Nitakuokoa kutoka kwa watu na watu wa Mataifa ambapo ninakutuma,
18 to open their eyes, to turn them from darkness unto light, and from the power of Satan unto God, in order that they may receive remission of sins, and an inheritance among those who are sanctified by faith in me.
kufungua macho yao na kuwatoa gizani kwenda kwenye mwanga na kutoka kwenye nguvu za shetani wamgeukie Mungu; ili wapate kupokea kutoka kwa Mungu msamaha wa dhambi na urithi ambao nimewapa wale niliowatenga kwa imani iliyo kwangu.
19 Therefore, O king, I was not disobedient to the heavenly vision:
Hivyo, mfalme Agripa, sikuweza kuasi maono ya mbinguni,
20 but first to those in Damascus, and also in Jerusalem, and throughout all the country of Judea, and to the Gentiles, I was preaching that they should repent and turn to God, doing things worthy of repentance.
lakini, kwa wale walio katika Dameski kwanza, na kisha Yerusalemu na nchi yote ya Yudea, na pia kwa watu wa mataifa mengine, nilihubiri kwamba watubu na kumgeukia Mungu, wafanye matendo yanayostahili toba.
21 On account of these things the Jews, taking me while in the temple, endeavored to kill me.
Kwa sababu hiyo Wayahudi walinikamata hekaluni, wakajaribu kuniua.
22 Then having received help from God, I have stood unto this day, witnessing both to small and great, saying nothing but what the prophets and Moses said were about to come to pass:
Mungu amenisaidia mpaka sasa, hivyo nasimama na kushuhudia kwa watu wa kawaida na kwa wale wakubwa juu ya yale ambayo manabii na Musa walisema yatatokea na si vingine;
23 how that Christ must suffer, how being the first from the resurrection of the dead, he is to proclaim light both to the people, and the Gentiles.
kwamba Kristo lazima atateseka na atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu na kutangaza mwanga kwa Wayahudi na watu wa mataifa.
24 And he making his defence to these things, Festus says with a loud voice, O Paul, thou art beside thyself; many writings turned thee into insanity.
Paulo alipomaliza kujitetea, Festo alisema kwa sauti kubwa, 'Paulo, wewe ni mwendawazimu! masomo yako yamekufanya uwe mwendawazimu.
25 But Paul says, I am not a maniac, most noble Festus; but I speak forth the words of truth and soberness.
Lakini Paulo akasema, Mimi si mwendawazimu, mheshimiwa Festo; lakini kwa ujasiri nasema maneno ya ukweli mtupu.
26 For the king, to whom I also speak boldly, knows concerning these things: for I am persuaded that nothing of these things is hidden; for this has not been done in a corner.
Kwa kuwa mfalme anajua kuhusu mambo haya; na hivyo, ninaongea kwa uhuru kwake, kwa maana nina hakika kwamba hakuna lolote lililofichwa kwake; kwa kuwa hili halijafanywa pembeni.
27 O king Agrippa, dost thou believe the prophets? I know that thou believest them.
Je, unaamini manabii, Mfalme Agripa? Najua kwamba unaamini. '
28 And Agrippa said to Paul, With little persuasion thou dost persuade thyself to make me a Christian.
Agripa akamwambia Paulo, 'Kwa muda mfupi unaweza kunishawishi mimi na kunifanya Mkristo?
29 And Paul said, I would to God, that both in little and in much, not only you, but also all of those hearing me this day, were such as I am, except these bonds.
Paulo akasema, '“Namwomba Mungu kwamba, kwa muda mfupi au mrefu, si wewe tu, bali pia wote wanaonisikia leo, wawe kama mimi, lakini bila hii minyororo ya gerezani.”
30 And the king, and the governor, and Bernice, and those sitting with them, arose up:
Ndipo mfalme alisimama, na liwali, na Bernike pia, na wale waliokuwa wamekaa pamoja nao,
31 and having gone away, they were talking to one another, saying, that This man is doing nothing worthy of death or of bonds.
walipoondoka ukumbini, walizungumzia wao kwa wao na kusema, 'Mtu huyu hastahili kifo wala kifungo.'
32 But Agrippa said to Festus, This man was able to have been released, if he had not appealed to Caesar.
Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeweza kuwekwa huru kama asingekata rufani kwa Kaisari.”