< 3 John 1 >

1 The elder to the beloved Gaius, whom I truly love with divine love.
Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2 Beloved, I pray that you may prosper concerning all things and be well, as your soul prospers.
Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3 I rejoice exceedingly, the brethren coming and witnessing to thy truth, as thou art walking about in truth.
Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4 I have no greater joy than this, that I may hear of my children walking about in truth.
Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5 Beloved, whatsoever faithful deed thou mayest do to the brethren, thou art also dispensing to the strangers,
Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6 who have witnessed to thy divine love before the church: whom you will do well, having sent forth worthily of God.
Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7 For the sake of his name they went out, receiving nothing from the Gentiles.
Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8 Therefore we ought to receive such, in order that we may be fellow-workers with the truth.
Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9 I wrote something to the church, but Diotrephes, loving the preeminence over them, does not receive us.
Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10 On account of this, if I may come, I will remember his works which he is doing, berating us with wicked speeches: and not content with these, he does not receive the brethren, and he prohibits them wishing to receive them, and casts them out of the church.
Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11 Beloved, imitate not the evil, but the good. The one doing good is of God: the one doing evil has not seen God.
Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12 To Demetrius it has been testified by all, and by the truth itself: and we also testify: and you know that our testimony is true.
Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13 Having many things to write to you, but I do not wish to write them to you with ink and paper:
Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14 but I hope to see you immediately, and mouth to mouth we will speak. Peace be unto you. The friends salute you; salute the friends by name.
Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.

< 3 John 1 >