< 2 Peter 3 >
1 I indeed, beloved, write unto you this second epistle; in which I stir up your pure mind by remembrance:
Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
2 to remember the words which have been spoken hitherto by the holy prophets, and the commandment of the Lord and Saviour by your apostles:
Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
3 knowing this first, that at the last days mockers will come forth in scoffing, walking according to their own lusts,
Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
4 and saying, Where is the promise of his coming? for from the day when the fathers fell asleep, all things remain as from the beginning of creation.
na kusema: “Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!”
5 For they willingly forget this, that the heavens were in the olden time, and the earth standing out of the water and through the water, by the word of God;
Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
6 by which the world at that time, being flooded with water, perished:
na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
7 but now the heavens and the earth have been kept according to the same word, being reserved for fire in the day of judgment and the destruction of the ungodly people.
Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
8 But let not this one thing be forgotten, beloved, that one day with the Lord is as a thousand years, and a thousand years as one day.
Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
9 The Lord is not slack concerning his promise, as some people count slackness; but is long-suffering for your sakes, not wishing that any should perish, but all come to repentance.
Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
10 But the day of the Lord will come like a thief; in which the heavens will pass away with a great noise, and the elements being scorched up will be dissolved, and the earth and the works in it will be burnt up.
Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
11 Then all these things being dissolved, what kind of people does it behoove you to be in holy deportment and godliness,
Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
12 looking for and hastening the coming of the day of God, in which the heavens being on fire will be dissolved, and the elements being scorched up are melted?
mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi—Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
13 But, according to his promises, we are looking for new heavens and a new earth, wherein righteousness dwells.
Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
14 Therefore, beloved, looking for these things, be diligent to be found spotless and blameless unto him in peace:
Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
15 and consider the longsuffering of the Lord's salvation; as our beloved brother Paul according to the wisdom which was given unto him has written unto you;
Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
16 as also in all his epistles, speaking in the same concerning these things; in which there are some things hard to understand, which the unlearned and unestablished wrest, as they also do the other scriptures, to their own destruction.
Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
17 Then you, beloved, foreknowing watch, lest, having been led away by the delusion of the ungodly, you may fall from your own stedfastness:
Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
18 but grow in the grace and knowledge of our Lord and Saviour Jesus Christ. To him be glory both now and unto the day of the age. (aiōn )
Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina. (aiōn )