< Zechariah 13 >

1 In that day there shall be a fountaine opened to the house of Dauid, and to the inhabitants of Ierusalem, for sinne and for vncleannesse.
Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
2 And in that day, sayth the Lord of hostes, I will cut off the names of the idoles out of the land: and they shall no more be remembred: and I will cause the prophets, and the vncleane spirit to depart out of the land.
Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
3 And when any shall yet prophesie, his father and his mother that begate him, shall say vnto him, Thou shalt not liue: for thou speakest lies in the name of the Lord: and his father and his mother that begat him, shall thrust him through, when he prophesieth.
Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
4 And in that day shall the prophetes be ashamed euery one of his vision, when he hath prophesied: neither shall they weare a rough garment to deceiue.
Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
5 But he shall say, I am no Prophet: I am an husbandman: for man taught me to be an heardman from my youth vp.
Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
6 And one shall say vnto him, What are these woundes in thine hands? Then he shall answere, Thus was I wounded in the house of my friendes.
Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
7 Arise, O sword, vpon my shepheard, and vpon the man, that is my fellow, sayth the Lord of hostes: smite the shepheard, and the sheepe shall be scattered: and I will turne mine hand vpon the litle ones.
Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
8 And in all the land, sayeth the Lord, two partes therein shall be cut off, and die: but the third shall be left therein.
Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
9 And I will bring that third part thorowe the fire, and will fine them as the siluer is fined, and will trye them as golde is tryed: they shall call on my Name, and I will heare them: I will say, It is my people, and they shall say, The Lord is my God.
Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”

< Zechariah 13 >