< Song of Solomon 5 >

1 I am come into my garden, my sister, my spouse: I gathered my myrrhe with my spice: I ate mine hony combe with mine hony, I dranke my wine with my milke: eate, O friends, drinke, and make you merie, O welbeloued.
Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na kikolezo changu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Marafiki Kuleni, enyi marafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
2 I sleepe, but mine heart waketh, it is the voyce of my welbeloued that knocketh, saying, Open vnto mee, my sister, my loue, my doue, my vndefiled: for mine head is full of dewe, and my lockes with the droppes of the night.
Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpenzi wangu, hua wangu, asiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
3 I haue put off my coate, howe shall I put it on? I haue washed my feete, howe shall I defile them?
Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
4 My welbeloued put in his hand by the hole of the doore, and mine heart was affectioned toward him.
Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
5 I rose vp to open to my welbeloued, and mine hands did drop downe myrrhe, and my fingers pure myrrhe vpon the handels of the barre.
Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
6 I opened to my welbeloued: but my welbeloued was gone, and past: mine heart was gone when hee did speake: I sought him, but I coulde not finde him: I called him, but hee answered mee not.
Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa amekwenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
7 The watchmen that went about the citie, founde me: they smote me and wounded me: the watchmen of the walles tooke away my vaile from me.
Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyangʼanya joho langu, hao walinzi wa kuta!
8 I charge you, O daughters of Ierusalem, if you finde my welbeloued, that you tell him that I am sicke of loue.
Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: kama mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
9 O the fairest among women, what is thy welbeloued more then other welbeloued? what is thy welbeloued more then another louer, that thou doest so charge vs?
Je, mpendwa wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpendwa wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
10 My welbeloued is white and ruddie, the chiefest of ten thousand.
Mpenzi wangu anangʼaa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
11 His head is as fine golde, his lockes curled, and blacke as a rauen.
Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
12 His eyes are like doues vpon the riuers of waters, which are washt with milke, and remaine by the full vessels.
Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
13 His cheekes are as a bedde of spices, and as sweete flowres, and his lippes like lilies dropping downe pure myrrhe.
Mashavu yake ni kama matuta ya vikolezo yakitoa manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
14 His hands as rings of gold set with the chrysolite, his belly like white yuorie couered with saphirs.
Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyongʼarishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
15 His legges are as pillars of marble, set vpon sockets of fine golde: his countenance as Lebanon, excellent as the cedars.
Miguu yake ni nguzo za marmar zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
16 His mouth is as sweete thinges, and hee is wholy delectable: this is my welbeloued, and this is my louer, O daughters of Ierusalem.
Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.

< Song of Solomon 5 >