< Ruth 4 >

1 Then went Boaz vp to the gate, and sate there, and beholde, the kinsman, of whome Boaz had spoken, came by: and he sayd, Ho, snch one, come, sit downe here. And he turned, and sate downe.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 Then he tooke ten men of the Elders of the citie, and sayd, Sit ye downe here. And they sate downe.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 And he said vnto ye kinsman, Naomi, that is come againe out of ye countrey of Moab, wil sell a parcel of land, which was our brother Elimelechs.
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 And I thought to aduertise thee, saying, Buy it before the assistants, and before the Elders of my people. If thou wilt redeeme it, redeeme it: but if thou wilt not redeeme it, tel me: for I know that there is none besides thee to redeeme it, and I am after thee. Then he answered, I wil redeeme it.
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 Then said Boaz, What day thou buyest the field of the hand of Naomi, thou mnst also buy it of Ruth the Moabitesse the wife of the dead, to stirre vp the name of the dead, vpon his inheritance.
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 And the kinsman answered, I can not redeeme it, lest I destroy mine owne inheritance: redeeme my right to thee, for I can not redeeme it.
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 Now this was the maner beforetime in Israel, concerning redeeming and changing, for to stablish all things: a man did plucke off his shooe, and gaue it his neighbour, and this was a sure witnes in Israel.
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 Therefore the kinsman sayd to Boas, Buy it for thee: and he drew off his shooe.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 And Boaz sayd vnto the Elders and vnto all the people, Ye are witnesses this day, that I haue bought all that was Elimelechs, and all that was Chilions and Mahlons, of the hand of Naomi.
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 And moreouer, Ruth the Moabitesse the wife of Mahlon, haue I bought to be my wife, to stirre vp the name of the dead vpon his inheritance, and that the name of the dead be not put out from among his brethren, and from the gate of his place: ye are witnesses this day.
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 And all the people that were in the gate, and the Elders sayd, We are witnesses: the Lord make the wife that commeth into thine house, like Rahel and like Leah, which twaine did build the house of Israel: and that thou mayest doe worthily in Ephrathah, and be famous in Beth-lehem,
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 And that thine house be like the house of Pharez (whom Thamar bare vnto Iudah) of the seede which the Lord shall giue thee of this yong woman.
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 So Boaz tooke Ruth, and she was his wife: and when he went in vnto her, the Lord gaue that she conceiued, and bare a sonne.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 And the women sayd vnto Naomi, Blessed be the Lord, which hath not left thee this day without a kinsman, and his name shalbe continued in Israel.
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 And this shall bring thy life againe, and cherish thine olde age: for thy daughter in lawe which loueth thee, hath borne vnto him, and she is better to thee then seuen sonnes.
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 And Naomi tooke the childe, and layde it in her lap, and became nource vnto it.
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 And the women her neighbours gaue it a name, saying, There is a childe borne to Naomi, and called the name thereof Obed: the same was the father of Ishai, the father of Dauid.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 These now are ye generations of Pharez: Pharez begate Hezron,
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 And Hezron begate Ram, and Ram begate Amminadab,
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 And Amminadab begate Nahshon, and Nahshon begate Salmah,
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 And Salmon begate Boaz, and Boaz begat Obed,
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 And Obed begate Ishai, and Ishai begate Dauid.
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.

< Ruth 4 >