< Romans 3 >
1 What is then the preferment of the Iewe? or what is the profite of circumcision?
Basi kuna faida gani kuwa Myahudi? Au kuna thamani gani katika tohara?
2 Much euery maner of way: for chiefly, because vnto them were of credite committed the oracles of God.
Kuna faida kubwa kwa kila namna! Kwanza kabisa, Wayahudi wamekabidhiwa lile Neno halisi la Mungu.
3 For what, though some did not beleeue? shall their vnbeliefe make the faith of God without effect?
Ingekuwaje kama wengine hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kungebatilisha uaminifu wa Mungu?
4 God forbid: yea, let God be true, and euery man a lyar, as it is written, That thou mightest be iustified in thy words, and ouercome, when thou art iudged.
La hasha! Mungu na aonekane mwenye haki, na kila mwanadamu kuwa mwongo, kama ilivyoandikwa: “Ili uthibitike kuwa wa kweli unaponena, na ukashinde utoapo hukumu.”
5 Now if our vnrighteousnes comend the righteousnes of God, what shall we say? Is God vnrighteous which punisheth? (I speake as a man.)
Ikiwa uovu wetu unathibitisha haki ya Mungu waziwazi, tuseme nini basi? Je, Mungu kuileta ghadhabu yake juu yetu ni kwamba yeye si mwenye haki? (Nanena kibinadamu.)
6 God forbid: els how shall God iudge ye world?
La hasha! Kama hivyo ndivyo ilivyo, Mungu angehukumuje ulimwengu?
7 For if the veritie of God hath more abounded through my lye vnto his glorie, why am I yet condemned as a sinner?
Mtu aweza kuuliza, “Kama uongo wangu unasaidia kuonyesha kweli ya Mungu na kuzidisha utukufu wake, kwa nini basi mimi nahukumiwa kuwa mwenye dhambi?”
8 And (as we are blamed, and as some affirme, that we say) why doe we not euil, that good may come thereof? whose damnation is iust.
Nasi kwa nini tusiseme, kama wengine wanavyotusingizia kuwa tunasema, “Tutende maovu ili mema yapate kuja?” Wao wanastahili hukumu yao.
9 What then? are we more excellent? No, in no wise: for we haue alreadie prooued, that all, both Iewes and Gentiles are vnder sinne,
Tusemeje basi? Je, sisi ni bora kuwaliko wao? La hasha! Kwa maana tumekwisha kuhakikisha kwa vyovyote kwamba Wayahudi na watu wa Mataifa wote wako chini ya nguvu ya dhambi.
10 As it is written, There is none righteous, no not one.
Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
11 There is none that vnderstandeth: there is none that seeketh God.
Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
12 They haue all gone out of the way: they haue bene made altogether vnprofitable: there is none that doeth good, no not one.
Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
13 Their throte is an open sepulchre: they haue vsed their tongues to deceit: the poyson of aspes is vnder their lippes.
“Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
14 Whose mouth is full of cursing and bitternesse.
“Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
15 Their feete are swift to shead blood.
“Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
16 Destruction and calamity are in their waies,
maangamizi na taabu viko katika njia zao,
17 And ye way of peace they haue not knowen.
wala njia ya amani hawaijui.”
18 The feare of God is not before their eies.
“Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
19 Now we know that whatsoeuer ye Lawe saieth, it saieth it to them which are vnder ye Law, that euery mouth may bee stopped, and all the world be subiect to the iudgement of God.
Basi tunajua ya kwamba chochote sheria inachosema, inawaambia wale walio chini ya sheria ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote uwajibike kwa Mungu.
20 Therefore by the woorkes of the Lawe shall no flesh be iustified in his sight: for by the Lawe commeth the knowledge of sinne.
Kwa hiyo hakuna binadamu hata mmoja atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria, kwa maana sheria hutufanya tuitambue dhambi.
21 But nowe is the righteousnesse, of God made manifest without the Lawe, hauing witnes of the Lawe and of the Prophets,
Lakini sasa, haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa pasipo sheria, ambayo Sheria na Manabii wanaishuhudia.
22 To wit, the righteousnesse of God by the faith of Iesus Christ, vnto all, and vpon all that beleeue.
Haki hii itokayo kwa Mungu hupatikana kwa Yesu Kristo kwa wote wamwaminio. Kwa maana hapo hakuna tofauti,
23 For there is no difference: for all haue sinned, and are depriued of the glorie of God,
kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,
24 And are iustified freely by his grace, through the redemption that is in Christ Iesus,
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
25 Whom God hath set forth to be a reconciliation through faith in his blood to declare his righteousnes, by the forgiuenesse of the sinnes that are passed,
Yeye ambaye Mungu alimtoa awe dhabihu ya upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alifanya hivi ili kuonyesha haki yake, kwa sababu kwa ustahimili wake aliziachilia zile dhambi zilizotangulia kufanywa.
26 Through the patience of God, to shewe at this time his righteousnesse, that hee might be iust, and a iustifier of him which is of the faith of Iesus.
Alifanya hivyo ili kuonyesha haki yake wakati huu, ili yeye awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yule anayemwamini Yesu.
27 Where is then the reioycing? It is excluded. By what Lawe? of woorkes? Nay: but by the Lawe of faith.
Basi, kujivuna kuko wapi? Kumewekwa mbali. Kwa sheria gani? Je, ni kwa ile ya matendo? La hasha, bali kwa ile sheria ya imani.
28 Therefore we conclude, that a man is iustified by faith, without the workes of the Lawe.
Kwa maana twaona kwamba mwanadamu huhesabiwa haki kwa njia ya imani wala si kwa matendo ya sheria.
29 God, is he the God of the Iewes onely, and not of the Gentiles also? Yes, euen of the Gentiles also.
Je, Mungu ni Mungu wa Wayahudi peke yao? Je, yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Naam, yeye ni Mungu wa watu wa Mataifa pia.
30 For it is one God, who shall iustifie circumcision of faith, and vncircumcision through faith.
Basi kwa kuwa tuna Mungu mmoja tu, atawahesabia haki wale waliotahiriwa kwa imani na wale wasiotahiriwa kwa imani iyo hiyo.
31 Doe we then make the Lawe of none effect through faith? God forbid: yea, we establish the Lawe.
Je, basi ni kwamba tunaibatilisha sheria kwa imani hii? La, hasha! Badala yake tunaithibitisha sheria.