< Revelation 9 >

1 And the fifth Angel blew the trumpet, and I saw a starre fall from heauen vnto the earth, and to him was giuen the key of the bottomlesse pit. (Abyssos g12)
Kisha malaika wa tano alipiga tarumbeta yake. Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka kwenye dunia. Nyota ilipewa ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
2 And he opened the bottomlesse pit, and there arose the smoke of the pit, as the smoke of a great fornace, and the sunne, and the ayre were darkened by the smoke of the pit. (Abyssos g12)
Alifungua shimo lisilo na kikomo, na moshi ukapanda juu kwa safu kutoka ndani ya shimo kama moshi kutoka katika tanuru kubwa. Jua na anga vilibadilika vikawa giza kwa sababu ya moshi uliotoka shimoni. (Abyssos g12)
3 And there came out of the smoke Locustes vpon the earth, and vnto them was giuen power, as the scorpions of the earth haue power.
Ndani ya moshi nzige walitoka kuja juu ya dunia, nao walipewa nguvu kama ile ya nge juu ya dunia.
4 And it was comanded them, that they should not hurt the grasse of the earth, neither any greene thing, neither any tree: but onely those men which haue not the seale of God in their foreheads.
Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti, isipokuwa tu watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao.
5 And to them was comanded that they should not kill them, but that they should be vexed fiue moneths, and that their paine should be as the paine that commeth of a scorpion, when he hath stung a man.
Hawakupewa ruhusa ya kuwaua hao watu, bali kuwatesa tu kwa miezi mitano. Uchungu wao ulikuwa kama ule wa kuumwa na nge amwumapo mtu.
6 Therefore in those dayes shall men seeke death, and shall not finde it, and shall desire to die, and death shall flie from them.
Katika siku hizo watu watatafuta kifo, lakini hawatakipata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 And the forme of the locustes was like vnto horses prepared vnto battel, and on their heads were as it were crownes, like vnto golde, and their faces were like the faces of men.
Nzige walifanana na farasi walioandaliwa kwa vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji ya dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 And they had heare as the heare of women, and their teeth were as the teeth of lyons.
Walikuwa na nywele kama za wanawake na meno yao yalikuwa kama ya simba.
9 And they had habbergions, like to habbergions of yron: and the soud of their wings was like the sound of charets whe many horses runne vnto battel.
Walikuwa na vifua kama vifua vya chuma na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari mengi ya vita na farasi wakimbiao kwenda vitani.
10 And they had tailes like vnto scorpions, and there were stings in their tailes, and their power was to hurt men fiue moneths.
Walikuwa na mikia inayouma kama nge; katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano.
11 And they haue a King ouer them, which is the Angel of the bottomlesse pit, whose name in Hebrewe is Abaddon, and in Greeke he is named Apollyon, that is, destroying. (Abyssos g12)
Walikuwa naye kama mfalme juu yao malaika wa shimo lisilokuwa na mwisho. Jina lake katika Kiebrania ni Abadoni, na katika Kiyunani ana jina Apolioni. (Abyssos g12)
12 One woe is past, and beholde, yet two woes come after this.
Ole ya kwanza imepita. Angalia! Baada ya hili kuna maafa mawili yaja.
13 Then the sixt Angel blew the trumpet, and I heard a voyce from the foure hornes of the golden altar, which is before God,
Malaika wa sita alipiga tarumbeta yake, na nikasikia sauti ikitoka katika pembe ya madhabahu ya dhahabu ambayo iko mbele za Mungu.
14 Saying to the sixt Angel, which had the trumpet, Loose the foure Angels, which are bound in the great riuer Euphrates.
Sauti ilimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta, “Waachie malaika wanne ambao wamefungwa katika mto mkubwa Efrata.”
15 And the foure Angels were loosed, which were prepared at an houre, at a day, at a moneth, and at a yeere, to slay the thirde part of men.
Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa saa hiyo maalumu, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo, waliachiwa wawaue theluthi ya wanadamu.
16 And the nomber of horsemen of warre were twentie thousand times ten thousand: for I heard the nomber of them.
Idadi ya maaskari waliokuwa juu ya farasi ilikuwa 200, 000, 000. Nilisikia idadi yao.
17 And thus I saw the horses in a vision, and them that sate on them, hauing firie habbergions, and of Iacinth, and of brimstone, and the heads of the horses were as the heades of lyons: and out of their mouthes went foorth fire and smoke and brimstone.
Hivi ndivyo nilivyoona farasi katika maono yangu na wale waliopanda juu yao: Vifua vyao vilikuwa vyekundu kama moto, bluu iliyoiva na njano isiyoiva. Vichwa vya farasi vilifanana na vichwa vya simba, na midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa.
18 Of these three was the thirde part of men killed, that is, of the fire, and of the smoke, and of the brimstone, which came out of their mouthes.
Theluthi ya wanadamu waliuawa na haya mapigo matatu: moto, moshi, na salfa iliyotoka katika midomo yao.
19 For their power is in their mouths, and in their tailes: for their tailes were like vnto serpents, and had heades, wherewith they hurt.
Kwa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao—kwa kuwa mikia yao ilikuwa kama nyoka, na walikuwa na vichwa ambavyo walitumia kuwatia majeraha wanadamu.
20 And the remnant of the men which were not killed by these plagues, repented not of the works of their handes that they should not worship deuils, and idoles of golde and of siluer, and of brasse, and of stone, and of wood, which neither can see, neither heare nor goe.
Watu waliobaki, wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya, hawakutubia matendo yao waliyokuwa wamefanya, wala hawakuacha kuabudu mapepo na miungu ya dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti—vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea.
21 Also they repented not of their murder, and of their sorcerie, neither of their fornication, nor of their theft.
Wala hawakutubia uuaji wao, uchawi wao, uasherati wao au njia zao za wizi.

< Revelation 9 >