< Revelation 7 >

1 And after that, I sawe foure Angels stand on the foure corners of the earth, holding the foure windes of the earth, that the winds should not blow on the earth, neither on the sea, neither on any tree.
Baada ya hayo nikawaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za dunia wakishika pepo nne za dunia ili upepo usivume hata kidogo: wala katika nchi, wala baharini, wala kwenye miti.
2 And I sawe another Angel come vp from the East, which had the seale of the liuing God, and hee cried with a loud voice to the foure Angels to who power was giuen to hurt the earth, and the sea, saying,
Kisha nikamwona malaika mwingine akipanda juu kutoka mashariki akiwa na mhuri wa Mungu aliye hai. Akapaaza sauti na kuwaambia hao malaika wanne waliokabidhiwa jukumu la kuiharibu nchi na bahari,
3 Hurt ye not the earth, neither the sea, neither the trees, til we haue sealed the seruants of our God in their foreheads.
“Msiharibu nchi, wala bahari, wala miti, mpaka tutakapokwisha wapiga mhuri watumishi wa Mungu wetu katika paji la uso.”
4 And I heard the number of them, which were sealed, and there were sealed an hundreth and foure and fourtie thousand of all the tribes of the children of Israel.
Kisha nikasikia idadi ya hao waliopigwa mhuri: Watu mia moja arobaini na nne elfu wa makabila yote ya watu wa Israeli.
5 Of the tribe of Iuda were sealed twelue thousande. Of the tribe of Ruben were sealed twelue thousande. Of the tribe of Gad were sealed twelue thousande.
Kabila la Yuda walikuwa watu kumi na mbili elfu; kabila la Reubeni, kumi na mbili elfu, kabila la Gadi, kumi na mbili elfu;
6 Of the tribe of Aser were sealed twelue thousand. Of the tribe of Nephthali were sealed twelue thousand. Of the tribe of Manasses were sealed twelue thousand.
Kabila la Asheri, kumi na mbili elfu; kabila la Naftali, kumi na mbili elfu; kabila la Manase, kumi na mbili elfu;
7 Of the tribe of Simeon were sealed twelue thousande. Of the tribe of Leui were sealed twelue thousande. Of the tribe of Issachar were sealed twelue thousand. Of the tribe of Zabulon were sealed twelue thousand.
kabila la Simeoni, kumi na mbili elfu, kabila la Lawi, kumi na mbili elfu, kabila la Isakari, kumi na mbili elfu;
8 Of the tribe of Ioseph were sealed twelue thousande. Of the tribe of Beniamin were sealed twelue thousand.
kabila la Zabuloni, kumi na mbili elfu; kabila la Yosefu, kumi na mbili elfu, na kabila la Benyamini, kumi na mbili elfu.
9 After these thinges I behelde, and loe a great multitude, which no man coulde number, of all nations and kindreds, and people, and tongues, stoode before the throne, and before the Lambe, clothed with long white robes, and palmes in their hands.
Kisha nikatazama, nikaona umati mkubwa wa watu wasiohesabika: watu wa kila taifa, ukoo, jamaa na lugha. Nao walikuwa wamesimama mbele ya kiti cha enzi na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa mavazi meupe na kushika matawi ya mitende mikononi mwao.
10 And they cried with a loud voice, saying, Saluation commeth of our God, that sitteth vpon the throne, and of the Lambe.
Wakapaaza sauti: “Ukombozi wetu watoka kwa Mungu wetu aketiye juu ya kiti cha enzi, na kutoka kwa Mwanakondoo!”
11 And all the Angels stoode rounde about the throne, and about the Elders, and the foure beastes, and they fell before the throne on their faces, and worshipped God,
Malaika wote wakasimama kukizunguka kiti cha enzi, wazee na vile viumbe hai vinne. Wakaanguka kifudifudi mbele ya kiti cha enzi, wakamwabudu Mungu,
12 Saying, Amen. Praise, and glorie, and wisdom, and thankes, and honour, and power, and might bee vnto our God for euermore, Amen. (aiōn g165)
wakisema, “Amina! Sifa, utukufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu, milele na milele! Amina!” (aiōn g165)
13 And one of the Elders spake, saying vnto me, What are these which are araied in log white robes? and whence came they?
Mmoja wa hao wazee akaniuliza, “Hawa waliovaa mavazi meupe ni watu gani? Na wametoka wapi?”
14 And I saide vnto him, Lord, thou knowest. And he saide to me, These are they, which came out of great tribulation, and haue washed their long robes, and haue made their long robes white in the blood of the Lambe.
Nami nikamjibu, “Mheshimiwa, wewe wajua!” Naye akaniambia, “Hawa ni wale waliopita salama katika ule udhalimu mkuu. Waliyaosha mavazi yao katika damu ya Mwanakondoo, yakawa meupe kabisa.
15 Therefore are they in the presence of the throne of God, and serue him day and night in his Temple, and he that sitteth on the throne, wil dwell among them.
Ndiyo maana wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Humtumikia Mungu mchana na usiku katika Hekalu lake; naye aketiye juu ya kiti cha enzi atatandaza hema lake juu yao kuwalinda.
16 They shall hunger no more, neither thirst any more, neither shall the sunne light on them, neither any heate.
Hawataona tena njaa wala kiu; jua wala joto kali halitawachoma tena,
17 For the Lambe, which is in the middes of the throne, shall gouerne them, and shall leade them vnto the liuely fountaines of waters, and God shall wipe away all teares from their eyes.
kwa sababu Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi atakuwa mchungaji wao, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji ya uzima. Naye Mungu atayafuta machozi yote machoni mwao.”

< Revelation 7 >