< Revelation 21 >

1 And I sawe a newe heauen, and a newe earth: for the first heauen, and the first earth were passed away, and there was no more sea.
Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa kuwa mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza zimekwishapita, na bahari haikuwepo tena.
2 And I Iohn sawe the holie citie newe Hierusalem come downe from God out of heauen, prepared as a bride trimmed for her husband.
Niliona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ambao ulikuja chini kutoka mbinguni kwa Mungu, ulioandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
3 And I heard a great voice out of heauen, saying, Behold, the Tabernacle of God is with men, and he will dwell with them: and they shalbe his people, and God himselfe shalbe their God with them.
Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa nao na atakuwa Mungu wao.
4 And God shall wipe away all teares from their eyes: and there shalbe no more death, neither sorow, neither crying, neither shall there be any more paine: for the first things are passed.
Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na hapatakuwa na kifo tena, au kuomboleza, au kulia, au maumivu. Mambo ya zamani yamekwishakupita.
5 And he that sate vpon the throne, sayd, Behold, I make all things newe: and he sayde vnto me, Write: for these wordes are faithfull and true.
Yeye ambaye alikuwa ameketi juu ya kiti cha enzi alisema, “Tazama! Nafanya mambo yote kuwa mapya.” Alisema, “Andika hili kwa sababu maneno haya ni ya hakika na kweli.”
6 And he said vnto me, It is done, I am Alpha and Omega, the beginning and the ende. I wil giue to him that is a thirst, of the well of the water of life freely.
Aliniambia, “Mambo haya yalikwisha kupita! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kwa yeyote aonaye kiu nitampatia kinywaji bila gharama kutoka katika chemchemi za maji ya uzima.
7 He that ouercommeth, shall inherit all things, and I will be his God, and he shall be my sonne.
Yeye ashindaye atayarithi mambo haya, na nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 But the fearful and vnbeleeuing, and the abominable and murtherers, and whoremogers, and sorcerers, and idolaters, and all liars shall haue their part in the lake, which burneth with fire and brimstone, which is the second death. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Lakini kama ilivyo kwa waoga, wasioamini, wachukizao, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, sehemu yao itakuwa katika ziwa la moto wa kiberiti uunguzao. Hiyo ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 And there came vnto mee one of the seuen Angels, which had the seuen vials full of the seuen last plagues, and talked with mee, saying, Come: I will shewe thee the bride, the Lambes wife.
Mmoja wa malaika saba alikuja kwangu, mmoja ambaye alikuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho na alisema, “Njoo hapa. Nitakuonesha bibi harusi, mke wa mwana kondoo.”
10 And he caried me away in the spirit to a great: and an hie mountaine, and he shewed me that great citie, that holie Hierusalem, descending out of heauen from God,
Kisha alinichukua mbali katika Roho kwenye mlima mkubwa na mrefu na alinionesha mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka chini kutoka mbinguni kwa Mungu.
11 Hauing the glorie of God: and her shining was like vnto a stone most precious, as a Iasper stone cleare as crystall,
Yerusalemu ulikuwa na utukufu wa Mungu, na uzuri wake ulikuwa kama kito cha thamani, kama jiwe la kioo safi la yaspi.
12 And had a great wall and hie, and had twelue gates, and at the gates twelue Angels, and the names written, which are the twelue tribes of the children of Israel.
Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye milango kumi na miwili, pamoja na malaika kumi na wawili milangoni. Juu ya milango palikuwa pameandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.
13 On the East part there were three gates, and on the Northside three gates, on the Southside three gates, and on the Westside three gates.
Upande wa mashariki palikuwa na milango mitatu, upande wa kusini milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, na upande wa magharibi milango mitatu.
14 And the wall of the citie had twelue foundations, and in them the Names of the Lambes twelue Apostles.
Kuta za mji zilikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake palikuwa na majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana Kondoo.
15 And hee that talked with mee, had a golden reede, to measure the citie withall, and the gates thereof, and the wall thereof.
Mmoja aliyeongea nami alikuwa na kipimo cha fimbo iliyotengenezwa kwa dhahabu kwa ajili ya kupima mji, milango yake na kuta zake.
16 And the citie laie foure square, and the length is as large as the bredth of it, and he measured the citie with the reede, twelue thousande furlongs: and the length, and the bredth, and the height of it are equall.
Mji uliwekwa ndani ya mraba; urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Alipima mji kwa kipimio cha fimbo, stadia 12, 000 kwa urefu (urefu wake, upana, na kimo vilifanana).
17 And hee measured the wall thereof, an hundreth fourtie and foure cubites, by the measure of man, that is, of the Angell.
Vilevile alipima ukuta wake, unene wake ulikuwa dhiraa 144 kwa vipimo vya kibinadamu (ambavyo pia ni vipimo vya malaika).
18 And ye building of the wall of it was of Iasper: and the citie was pure golde, like vnto cleare glasse.
Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji wenye dhahabu safi, kama kioo safi.
19 And the foundations of the wall of ye city were garnished with all maner of precious stones: the first foundation was Iasper: the second of Saphire: the third of a Chalcedonie: the fourth of an Emeraude:
Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa na kila aina ya jiwe la thamani. La kwanza lilikuwa yaspi, la pili lilikuwa yakuti samawi, la tatu lilikuwa kalkedon, la nne zumaridi,
20 The fift of a Sardonix: the sixt of a Sardius: the seueth of a Chrysolite: the eight of a Beryl: the ninth of a Topaze: the tenth of a Chrysoprasus: the eleuenth of a Iacynth: the twelfth an Amethyst.
la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolitho, la nane zabarajadi, la tisa yakuti ya manjano, la kumi krisopraso, la kumi na moja hiakintho, la kumi na mbili amethisto.
21 And the twelue gates were twelue pearles, and euery gate is of one pearle, and the streete of the citie is pure golde, as shining glasse.
Milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili, kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja. Mitaa ya mji ilikuwa dhahabu safi, ikionekana kama kioo safi.
22 And I sawe no Temple therein: for the Lord God almightie and the Lambe are the Temple of it.
Sikuona hekalu lolote ndani ya mji, kwa kuwa Bwana Mungu, ambaye anatawala juu ya vyote, na Mwana Kondoo ni hekalu lake.
23 And this citie hath no neede of the sunne, neither of the moone to shine in it: for the glorie of God did light it: and the Lambe is the light of it.
Mji haukuhitaji jua au mwezi ili kungaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu uliangaza juu yake, na taa yake ni Mwana Kondoo.
24 And the people which are saued, shall walke in the light of it: and the Kings of the earth shall bring their glorie and honour vnto it.
Mataifa watatembea kwa mwanga wa mji huo. Wafalme wa dunia wataleta fahari zao ndani yake.
25 And the gates of it shall not be shut by day: for there shalbe no night there.
Milango yake haitafungwa wakati wa mchana, na hapatakuwa na usiku pale.
26 And the glorie, and honour of the Gentiles shall be brought vnto it.
Wataleta fahari na heshima ya mataifa ndani yake,
27 And there shall enter into it none vncleane thing, neither whatsoeuer woorketh abomination or lies: but they which are written in ye Lambes booke of life.
na hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake. Wala yeyote ambaye afanyaye jambo lolote la aibu au udanganyifu hataingia, bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana Kondoo.

< Revelation 21 >