< Revelation 1 >
1 The Reuelation of Iesus Christ, which God gaue vnto him, to shewe vnto his seruants things which must shortly be done: which he sent, and shewed by his Angel vnto his seruant Iohn,
Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2 Who bare record of ye word of God, and of the testimonie of Iesus Christ, and of all things that he saw.
naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3 Blessed is he that readeth, and they that heare the wordes of this prophecie, and keepe those things which are written therein: for the time is at hand.
Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4 Iohn, to the seuen Churches which are in Asia, Grace be with you, and peace from him, Which is, and Which was, and Which is to come, and from the seuen Spirits which are before his Throne,
Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5 And from Iesus Christ, which is that faithful witnes, and that first begotten of the dead, and that Prince of the Kings of the earth, vnto him that loued vs, and washed vs from our sinnes in his blood,
na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6 And made vs Kings and Priests vnto God euen his Father, to him I say be glory, and dominion for euermore, Amen. (aiōn )
akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. (aiōn )
7 Beholde, he commeth with cloudes, and euery eye shall see him: yea, euen they which pearced him thorowe: and all kinreds of the earth shall waile before him, Euen so, Amen.
Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8 I am Alpha and Omega, the beginning and the ending, saith the Lord, Which is, and Which was, and Which is to come, euen the Almightie.
“Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9 I Iohn, euen your brother, and companion in tribulation, and in the kingdome and patience of Iesus Christ, was in the yle called Patmos, for the worde of God, and for the witnessing of Iesus Christ.
Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10 And I was rauished in spirit on the Lordes day, and heard behinde me a great voyce, as it had bene of a trumpet,
Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11 Saying, I am Alpha and Omega, that first and that last: and that which thou seest, write in a booke, and send it vnto the seuen Churches which are in Asia, vnto Ephesus, and vnto Smyrna, and vnto Pergamus, and vnto Thyatira, and vnto Sardis, and vnto Philadelphia, and vnto Laodicea.
Nayo ilisema, “Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea.”
12 Then I turned backe to see the voyce, that spake with me: and when I was turned, I sawe seuen golden candlestickes,
Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13 And in the middes of the seuen candlestickes, one like vnto the Sonne of man, clothed with a garment downe to the feete, and girded about the pappes with a golden girdle.
na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14 His head, and heares were white as white wooll, and as snowe, and his eyes were as a flame of fire,
Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15 And his feete like vnto fine brasse, burning as in a fornace: and his voyce as the sounde of many waters.
miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16 And he had in his right hand seuen starres: and out of his mouth went a sharpe two edged sword: and his face shone as the sunne shineth in his strength.
Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17 And when I saw him, I fell at his feete as dead: then he laid his right hand vpon me, saying vnto me, Feare not: I am that first and that last,
Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18 And am aliue, but I was dead: and beholde, I am aliue for euermore, Amen: and I haue the keyes of hell and of death. (aiōn , Hadēs )
Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu. (aiōn , Hadēs )
19 Write the things which thou hast seene, and the things which are, and the things which shall come hereafter.
Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20 The misterie of the seuen starres which thou sawest in my right hand, and the seuen golden candlestickes, is this, The seuen starres are the Angels of the seuen Churches: and the seuen candlestickes which thou sawest, are the seuen Churches.
Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.