< Psalms 1 >

1 Blessed is the man that doeth not walke in the counsell of the wicked, nor stand in the way of sinners, nor sit in ye seate of the scornefull:
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 But his delite is in the Lawe of the Lord, and in his Lawe doeth he meditate day and night.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 For he shall be like a tree planted by the riuers of waters, that will bring foorth her fruite in due season: whose leafe shall not fade: so whatsoeuer he shall doe, shall prosper.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 The wicked are not so, but as the chaffe, which the winde driueth away.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stande in the iudgement, nor sinners in the assemblie of the righteous.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the Lord knoweth the way of the righteous, and the way of the wicked shall perish.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Psalms 1 >