< Psalms 87 >
1 A Psalme or song committed to the sonnes of Korah. God layde his foundations among the holy mountaines.
Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 The Lord loueth the gates of Zion aboue all the habitations of Iaakob.
Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
3 Glorious things are spoken of thee, O citie of God. (Selah)
Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
4 I will make mention of Rahab and Babel among them that knowe me: beholde Palestina and Tyrus with Ethiopia, There is he borne.
“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
5 And of Zion it shall be sayde, Many are borne in her: and he, euen the most High shall stablish her.
Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
6 The Lord shall count, when hee writeth the people, He was borne there. (Selah)
Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 Aswell the singers as the players on instruments shall prayse thee: all my springs are in thee.
Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”