< Psalms 78 >
1 A Psalme to give instruction committed to Asaph. Heare my doctrine, O my people: incline your eares vnto the wordes of my mouth.
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I will open my mouth in a parable: I will declare high sentences of olde.
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Which we haue heard and knowen, and our fathers haue tolde vs.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Wee will not hide them from their children but to the generation to come we wil shewe the praises of the Lord his power also, and his wonderful woorkes that he hath done:
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 How he established a testimonie in Iaakob, and ordeined a Law in Israel, which he commanded our fathers, that they shoulde teache their children:
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 That the posteritie might knowe it, and the children, which should be borne, should stand vp, and declare it to their children:
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 That they might set their hope on God, and not forget the workes of God but keepe his commandements:
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 And not to bee as their fathers, a disobedient and rebellious generation: a generation that set not their heart aright, and whose spirite was not faithfull vnto God.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 The children of Ephraim being armed and shooting with the bowe, turned backe in the day of battell.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 They kept not the couenant of God, but refused to walke in his Lawe,
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 And forgate his Actes, and his wonderfull woorkes that he had shewed them.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Hee did marueilous thinges in the sight of their fathers in the lande of Egypt: euen in the fielde of Zoan.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 He deuided the Sea, and led them through: he made also the waters to stand as an heape.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 In the day time also hee led them with a cloude, and all the night with a light of fire.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 He claue the rockes in the wildernes, and gaue them drinke as of the great depths.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 He brought floods also out of the stonie rocke; so that hee made the waters to descend like the riuers.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Yet they sinned stil against him, and prouoked the Highest in the wildernesse,
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 And tempted God in their heartes in requiring meate for their lust.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 They spake against God also, saying, Can God prepare a table in the wildernesse?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Behold, he smote the rocke, that the water gushed out, and the streames ouerflowed: can hee giue bread also? or prepare flesh for his people?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Therefore the Lord heard and was angrie, and the fire was kindled in Iaakob, and also wrath came vpon Israel,
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Because they beleeued not in God, and trusted not in his helpe.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Yet he had comanded the clouds aboue, and had opened the doores of heauen,
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 And had rained downe MAN vpon them for to eate, and had giuen them of the wheate of heauen.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Man did eate the bread of Angels: hee sent them meate ynough.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 He caused the Eastwinde to passe in the heauen, and through his power he brought in the Southwinde.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 Hee rained flesh also vpon them as dust, and feathered foule as the sand of the sea.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 And hee made it fall in the middes of their campe euen round about their habitations.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 So they did eate and were well filled: for he gaue them their desire.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 They were not turned from their lust, but the meate was yet in their mouthes,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 When the wrath of God came euen vpon them, and slew the strongest of them, and smote downe the chosen men in Israel.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 For all this, they sinned stil, and beleeued not his wonderous woorkes.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Therefore their daies did hee consume in vanitie, and their yeeres hastily.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 And when hee slewe them, they sought him and they returned, and sought God earely.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 And they remembred that God was their strength, and the most high God their redeemer.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 But they flattered him with their mouth, and dissembled with him with their tongue.
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 For their heart was not vpright with him: neither were they faithfull in his couenant.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Yet he being merciful forgaue their iniquitie, and destroied them not, but oft times called backe his anger, and did not stirre vp all his wrath.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 For he remembered that they were flesh: yea, a winde that passeth and commeth not againe.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 How oft did they prouoke him in the wildernes? and grieue him in the desert?
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Yea, they returned, and tempted God, and limited the Holie one of Israel.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 They remembered not his hand, nor the day when he deliuered them from the enemie,
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 Nor him that set his signes in Egypt, and his wonders in the fielde of Zoan,
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 And turned their riuers into blood, and their floods, that they could not drinke.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Hee sent a swarme of flies among them, which deuoured them, and frogs, which destroyed them.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 He gaue also their fruites vnto the caterpiller, and their labour vnto the grassehopper.
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 He destroied their vines with haile, and their wilde figge trees with the hailestone.
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 He gaue their cattell also to the haile, and their flockes to the thunderboltes.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 Hee cast vpon them the fiercenesse of his anger, indignation and wrath, and vexation by the sending out of euill Angels.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 He made a way to his anger: he spared not their soule from death, but gaue their life to the pestilence,
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 And smote al the firstborne in Egypt, euen the beginning of their strength in the tabernacles of Ham.
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 But hee made his people to goe out like sheepe, and led them in the wildernes like a flocke.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Yea, he caried them out safely, and they feared not, and the Sea couered their enemies.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 And he brought them vnto the borders of his Sanctuarie: euen to this Mountaine, which his right hand purchased.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 He cast out the heathe also before them, and caused them to fall to the lot of his inheritance, and made the tribes of Israel to dwell in their tabernacles.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Yet they tempted, and prouoked the most high God, and kept not his testimonies,
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 But turned backe and delt falsely like their fathers: they turned like a deceitfull bowe.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 And they prouoked him to anger with their high places, and mooued him to wrath with their grauen images.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 God heard this and was wroth, and greatly abhorred Israel,
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 So that hee forsooke the habitation of Shilo, euen the Tabernacle where hee dwelt among men,
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 And deliuered his power into captiuitie, and his beautie into the enemies hand.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 And hee gaue vp his people to the sworde, and was angrie with his inheritance.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 The fire deuoured their chosen men, and their maides were not praised.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Their Priestes fell by the sworde, and their widowes lamented not.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 But the Lord awaked as one out of sleepe, and as a strong man that after his wine crieth out,
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 And smote his enemies in the hinder parts, and put them to a perpetuall shame.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Yet he refused the tabernacle of Ioseph, and chose not the tribe of Ephraim:
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 But chose the tribe of Iudah, and mount Zion which he loued.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 And he built his Sanctuarie as an high palace, like the earth, which he stablished for euer.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 He chose Dauid also his seruant, and tooke him from the shepefolds.
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 Euen from behinde the ewes with yong brought he him to feede his people in Iaakob, and his inheritance in Israel.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 So he fed them according to the simplicitie of his heart, and guided them by the discretion of his hands.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.