< Psalms 75 >

1 To him that excelleth. Destroy not. A Psalme or song committed toAsaph. We will prayse thee, O God, we will prayse thee, for thy Name is neere: therefore they will declare thy wonderous workes.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 When I shall take a conuenient time, I will iudge righteously.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 The earth and all the inhabitantes thereof are dissolued: but I will establish the pillars of it. (Selah)
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 I saide vnto the foolish, Be not so foolish, and to the wicked, Lift not vp the horne.
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Lift not vp your horne on high, neither speake with a stiffe necke.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 For to come to preferment is neither from the East, nor from the West, nor from the South,
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 But God is the iudge: he maketh lowe and he maketh hie.
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 For in the hand of the Lord is a cup, and the wine is red: it is full mixt, and he powreth out of the same: surely all the wicked of the earth shall wring out and drinke the dregges thereof.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 But I will declare for euer, and sing prayses vnto the God of Iaakob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 All the hornes of the wicked also will I breake: but the hornes of the righteous shalbe exalted.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psalms 75 >