< Psalms 64 >

1 To him that excelleth. A Psalme of David. Heare my voyce, O God, in my prayer: preserue my life from feare of the enemie.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 Hide me from the conspiracie of the wicked, and from the rage of the workers of iniquitie.
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 Which haue whette their tongue like a sword, and shot for their arrowes bitter wordes.
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 To shoote at the vpright in secrete: they shoote at him suddenly, and feare not.
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
5 They encourage themselues in a wicked purpose: they commune together to lay snares priuilie, and say, Who shall see them?
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 They haue sought out iniquities, and haue accomplished that which they sought out, euen euery one his secret thoughtes, and the depth of his heart.
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 But God will shoote an arrowe at them suddenly: their strokes shalbe at once.
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
8 They shall cause their owne tongue to fall vpon them: and whosoeuer shall see them, shall flee away.
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
9 And all men shall see it, and declare the worke of God, and they shall vnderstand, what he hath wrought.
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 But the righteous shall be glad in the Lord, and trust in him: and all that are vpright of heart, shall reioyce.
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< Psalms 64 >