< Psalms 57 >
1 To him that excelleth. Destroy not. A Psalme of David on Michtam. When he fled from Saul in the cave. Have mercie vpon me, O God, haue mercie vpon me: for my soule trusteth in thee, and in the shadowe of thy wings wil I trust, till these afflictions ouerpasse.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 I will call vnto the most high God, euen to the God, that performeth his promise toward me.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 He will send from heauen, and saue me from the reproofe of him that would swallowe me. (Selah) God wil send his mercy, and his trueth.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 My soule is among lions: I lie among the children of men, that are set on fire: whose teeth are speares and arrowes, and their tongue a sharpe sworde.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Exalt thy selfe, O God, aboue the heauen, and let thy glory be vpon all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 They haue layd a net for my steps: my soule is pressed downe: they haue digged a pit before me, and are fallen into the mids of it. (Selah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 Mine heart is prepared, O God, mine heart is prepared: I will sing and giue prayse.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Awake my tongue, awake viole and harpe: I wil awake early.
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 I will prayse thee, O Lord, among the people, and I wil sing vnto thee among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 For thy mercie is great vnto the heauens, and thy trueth vnto the cloudes.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Exalt thy selfe, O God, aboue the heauens, and let thy glory be vpon all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.