< Psalms 56 >
1 To him that excelleth. A Psalme of David on Michtam, concerning the dumme doue in a farre countrey, when the Philistims tooke him in Gath. Be mercifull vnto me, O God, for man would swallow me vp: he fighteth continually and vexeth me.
Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2 Mine enemies would dayly swallowe mee vp: for many fight against me, O thou most High.
Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3 When I was afrayd, I trusted in thee.
Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4 I will reioyce in God, because of his word, I trust in God, and will not feare what flesh can doe vnto me.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5 Mine owne wordes grieue me dayly: all their thoughtes are against me to doe me hurt.
Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6 They gather together, and keepe them selues close: they marke my steps, because they waite for my soule.
Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
7 They thinke they shall escape by iniquitie: O God, cast these people downe in thine anger.
Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
8 Thou hast counted my wandrings: put my teares into thy bottel: are they not in thy register?
Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
9 When I cry, then mine enemies shall turne backe: this I know, for God is with me.
Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
10 I will reioyce in God because of his worde: in the Lord wil I reioyce because of his worde.
Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
11 In God doe I trust: I will not be afrayd what man can doe vnto me.
katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
12 Thy vowes are vpon me, O God: I will render prayses vnto thee.
Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
13 For thou hast deliuered my soule from death, and also my feete from falling, that I may walke before God in the light of the liuing.
Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.