< Psalms 44 >

1 To him that excelleth. A Psalme to give instruction, committed to the sonnes of Korah. We haue heard with our eares, O God: our fathers haue tolde vs the workes, that thou hast done in their dayes, in the olde time:
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 Howe thou hast driuen out the heathen with thine hand, and planted them: how thou hast destroyed the people, and caused them to grow.
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 For they inherited not the lande by their owne sworde, neither did their owne arme saue them: but thy right hand, and thine arme and the light of thy countenance, because thou didest fauour them.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 Thou art my King, O God: send helpe vnto Iaakob.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 Through thee haue we thrust backe our aduersaries: by thy Name haue we troden downe them that rose vp against vs.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 For I do not trust in my bowe, neither can my sworde saue me.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 But thou hast saued vs from our aduersaries, and hast put them to confusion that hate vs.
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 Therefore will wee praise God continually, and will confesse thy Name for euer. (Selah)
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 But now thou art farre off, and puttest vs to confusion, and goest not forth with our armies.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 Thou makest vs to turne backe from the aduersary, and they, which hate vs, spoile for theselues.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 Thou giuest vs as sheepe to bee eaten, and doest scatter vs among the nations.
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 Thou sellest thy people without gaine, and doest not increase their price.
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 Thou makest vs a reproche to our neighbours, a iest and a laughing stocke to them that are round about vs.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 Thou makest vs a prouerbe among the nations, and a nodding of the head among the people.
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 My confusion is dayly before me, and the shame of my face hath couered me,
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 For the voyce of the slaunderer and rebuker, for the enemie and auenger.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All this is come vpon vs, yet doe wee not forget thee, neither deale wee falsly concerning thy couenant.
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Our heart is not turned backe: neither our steps gone out of thy paths,
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Albeit thou hast smitten vs downe into the place of dragons, and couered vs with the shadow of death.
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 If wee haue forgotten the Name of our God, and holden vp our hands to a strange god,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 Shall not God searche this out? for hee knoweth the secrets of the heart.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Surely for thy sake are we slaine continually, and are counted as sheepe for the slaughter.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Vp, why sleepest thou, O Lord? awake, be not farre off for euer.
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Wherefore hidest thou thy face? and forgettest our miserie and our affliction?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 For our soule is beaten downe vnto the dust: our belly cleaueth vnto the ground.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Rise vp for our succour, and redeeme vs for thy mercies sake.
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >