< Psalms 28 >

1 A Psalme of David. Unto thee, O Lord, doe I crie: O my strength, be not deafe toward mee, lest, if thou answere me not, I be like them that goe downe into the pit.
Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Heare the voyce of my petitions, when I crie vnto thee, when I holde vp mine handes towarde thine holy Oracle.
Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Drawe mee not away with the wicked, and with the woorkers of iniquitie: which speake friendly to their neighbours, when malice is in their hearts.
Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Reward them according to their deedes, and according to the wickednes of their inuentions: recompense them after the woorke of their handes: render them their reward.
Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
5 For they regarde not the woorkes of the Lord, nor the operation of his handes: therefore breake them downe, and builde them not vp.
Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
6 Praised be the Lord, for he hath heard the voyce of my petitions.
Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
7 The Lord is my strength and my shielde: mine heart trusted in him, and I was helped: therfore mine heart shall reioyce, and with my song will I praise him.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 The Lord is their strength, and he is the strength of the deliuerances of his anointed.
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Saue thy people, and blesse thine inheritance: feede them also, and exalt them for euer.
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

< Psalms 28 >