< Psalms 22 >
1 To him that excelleth upon Aiieleth Hasshahar. A Psalme of Dauid. My God, my God, why hast thou forsaken me, and art so farre from mine health, and from the wordes of my roaring?
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
2 O my God, I crie by day, but thou hearest not, and by night, but haue no audience.
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
3 But thou art holy, and doest inhabite the prayses of Israel.
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
4 Our fathers trusted in thee: they trusted, and thou didest deliuer them.
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
5 They called vpon thee, and were deliuered: they trusted in thee, and were not confounded.
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
6 But I am a worme, and not a man: a shame of men, and the contempt of the people.
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
7 All they that see me, haue me in derision: they make a mowe and nod the head, saying,
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
8 He trusted in the Lord, let him deliuer him: let him saue him, seeing he loueth him.
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
9 But thou didest draw me out of ye wombe: thou gauest me hope, euen at my mothers breasts.
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
10 I was cast vpon thee, euen from ye wombe: thou art my God from my mothers belly.
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11 Be not farre from me, because trouble is neere: for there is none to helpe me.
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12 Many yong bulles haue compassed me: mightie bulles of Bashan haue closed me about.
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13 They gape vpon me with their mouthes, as a ramping and roaring lyon.
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14 I am like water powred out, and all my bones are out of ioynt: mine heart is like waxe: it is molten in the middes of my bowels.
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15 My strength is dryed vp like a potsheard, and my tongue cleaueth to my iawes, and thou hast brought me into the dust of death.
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16 For dogges haue compassed me, and the assemblie of the wicked haue inclosed me: they perced mine hands and my feete.
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 I may tell all my bones: yet they beholde, and looke vpon me.
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18 They part my garments among them, and cast lottes vpon my vesture.
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19 But be thou not farre off, O Lord, my strength: hasten to helpe me.
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20 Deliuer my soule from the sword: my desolate soule from the power of the dogge.
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21 Saue me from the lyons mouth, and answere me in sauing me from the hornes of the vnicornes.
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22 I wil declare thy Name vnto my brethren: in the middes of the Congregation will I praise thee, saying,
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
23 Prayse the Lord, ye that feare him: magnifie ye him, all the seede of Iaakob, and feare ye him, all the seede of Israel.
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
24 For he hath not despised nor abhorred ye affliction of the poore: neither hath he hid his face from him, but when he called vnto him, he heard.
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
25 My prayse shalbe of thee in the great Congregation: my vowes will I perfourme before them that feare him.
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
26 The poore shall eate and be satisfied: they that seeke after the Lord, shall prayse him: your heart shall liue for euer.
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
27 All the endes of the worlde shall remember themselues, and turne to the Lord: and all the kinreds of the nations shall worship before thee.
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
28 For the kingdome is the Lords, and he ruleth among the nations.
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
29 All they that be fat in the earth, shall eate and worship: all they that go downe into the dust, shall bowe before him, euen he that cannot quicken his owne soule.
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
30 Their seede shall serue him: it shalbe counted vnto the Lord for a generation.
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
31 They shall come, and shall declare his righteousnesse vnto a people that shall be borne, because he hath done it.
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!