< Psalms 2 >

1 Why doe the heathen rage, and the people murmure in vaine?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 The Kings of the earth band themselues, and the princes are assembled together against the Lord, and against his Christ.
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 Let vs breake their bands, and cast their cordes from vs.
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 But he that dwelleth in the heauen, shall laugh: the Lord shall haue them in derision.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Then shall hee speake vnto them in his wrath, and vexe them in his sore displeasure, saying,
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 Euen I haue set my King vpon Zion mine holy mountaine.
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will declare the decree: that is, the Lord hath said vnto me, Thou art my Sonne: this day haue I begotten thee.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Aske of me, and I shall giue thee the heathen for thine inheritance, and the endes of the earth for thy possession.
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 Thou shalt krush them with a scepter of yron, and breake them in pieces like a potters vessell.
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Be wise nowe therefore, ye Kings: be learned ye Iudges of the earth.
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Serue the Lord in feare, and reioyce in trembling.
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Kisse the sonne, least he be angry, and ye perish in the way, when his wrath shall suddenly burne. blessed are all that trust in him.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Psalms 2 >