< Psalms 2 >
1 Why doe the heathen rage, and the people murmure in vaine?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 The Kings of the earth band themselues, and the princes are assembled together against the Lord, and against his Christ.
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 Let vs breake their bands, and cast their cordes from vs.
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 But he that dwelleth in the heauen, shall laugh: the Lord shall haue them in derision.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Then shall hee speake vnto them in his wrath, and vexe them in his sore displeasure, saying,
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Euen I haue set my King vpon Zion mine holy mountaine.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will declare the decree: that is, the Lord hath said vnto me, Thou art my Sonne: this day haue I begotten thee.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Aske of me, and I shall giue thee the heathen for thine inheritance, and the endes of the earth for thy possession.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Thou shalt krush them with a scepter of yron, and breake them in pieces like a potters vessell.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Be wise nowe therefore, ye Kings: be learned ye Iudges of the earth.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Serue the Lord in feare, and reioyce in trembling.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Kisse the sonne, least he be angry, and ye perish in the way, when his wrath shall suddenly burne. blessed are all that trust in him.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.