< Psalms 14 >

1 To him that excelleth. A Psalme of Dauid. The foole hath said in his heart, There is no God: they haue corrupted, and done an abominable worke: there is none that doeth good.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa; hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 The Lord looked downe from heauen vpon the children of men, to see if there were any that would vnderstand, and seeke God.
Bwana anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
3 All are gone out of the way: they are all corrupt: there is none that doeth good, no not one.
Wote wamepotoka, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
4 Doe not all the workers of iniquitie know that they eate vp my people, as they eate bread? they call not vpon the Lord.
Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Bwana?
5 There they shall be taken with feare, because God is in the generation of the iust.
Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 You haue made a mocke at the counsell of the poore, because the Lord is his trust.
Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini, bali Bwana ndiye kimbilio lao.
7 Oh giue saluation vnto Israel out of Zion: when the Lord turneth the captiuitie of his people, then Iaakob shall reioyce, and Israel shall be glad.
Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Bwana arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

< Psalms 14 >