< Psalms 135 >

1 Praise ye the Lord. Praise the Name of the Lord: ye seruants of the Lord, praise him.
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Ye that stande in the House of the Lord, and in the courtes of the House of our God,
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise ye the Lord: for the Lord is good: sing praises vnto his Name: for it is a comely thing.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 For the Lord hath chosen Iaakob to himselfe, and Israel for his chiefe treasure.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 For I know that the Lord is great, and that our Lord is aboue all gods.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Whatsoeuer pleased the Lord, that did hee in heauen and in earth, in the sea, and in all the depths.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 He bringeth vp the cloudes from the ends of the earth, and maketh the lightnings with ye raine: he draweth foorth the winde out of his treasures.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 He smote the first borne of Egypt both of man and beast.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 He hath sent tokens and wonders into the middes of thee, O Egypt, vpon Pharaoh, and vpon all his seruants.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 He smote many nations, and slew mightie Kings:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 As Sihon King of the Amorites, and Og King of Bashan, and all the kingdomes of Canaan:
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 And gaue their lande for an inheritance, euen an inheritance vnto Israel his people.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Thy Name, O Lord, endureth for euer: O Lord, thy remembrance is from generation to generation.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 For the Lord will iudge his people, and be pacified towardes his seruants.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 The idoles of the heathen are siluer and golde, euen the worke of mens handes.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 They haue a mouth, and speake not: they haue eyes and see not.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 They haue eares and heare not, neither is there any breath in their mouth.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 They that make them, are like vnto them: so are all that trust in them.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Praise the Lord, ye house of Israel: praise the Lord, ye house of Aaron.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Praise the Lord, ye house of Leui: ye that feare the Lord, praise the Lord.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Praised bee the Lord out of Zion, which dwelleth in Ierusalem. Praise ye the Lord.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalms 135 >