< Psalms 115 >
1 Not vnto vs, O Lord, not vnto vs, but vnto thy Name giue the glorie, for thy louing mercie and for thy truethes sake.
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Wherefore shall the heathen say, Where is nowe their God?
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 But our God is in heauen: he doeth what so euer he will.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Their idoles are siluer and golde, euen the worke of mens hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 They haue a mouth and speake not: they haue eyes and see not.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 They haue eares and heare not: they haue noses and smelll not.
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 They haue handes and touche not: they haue feete and walke not: neither make they a sound with their throte.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 They that make them are like vnto them: so are all that trust in them.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 O Israel, trust thou in the Lord: for he is their helpe and their shielde.
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 O house of Aaron, trust ye in the Lord: for he is their helpe and their shielde.
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 Ye that feare the Lord, trust in the Lord: for he is their helper and their shield.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 The Lord hath bene mindfull of vs: he will blesse, he will blesse the house of Israel, he will blesse the house of Aaron.
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 He will blesse them that feare the Lord, both small and great.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 The Lord will increase his graces towarde you, euen toward you and toward your children.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Ye are blessed of the Lord, which made the heauen and the earth.
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 The heauens, euen the heauens are the Lordes: but he hath giuen the earth to the sonnes of men.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 The dead prayse not the Lord, neither any that goe downe into the place of silence.
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 But we will prayse the Lord from henceforth and for euer. Prayse ye the Lord.
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.