< Psalms 113 >

1 Praise ye the Lord. Praise, O ye seruants of the Lord, prayse the Name of the Lord.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
2 Blessed be the Name of the Lord from hencefoorth and for euer.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
3 The Lordes Name is praysed from the rising of ye sunne, vnto ye going downe of the same.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 The Lord is high aboue all nations, and his glorie aboue the heauens.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
5 Who is like vnto the Lord our God, that hath his dwelling on high!
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 Who abaseth himselfe to beholde things in the heauen and in the earth!
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
7 He raiseth the needie out of the dust, and lifteth vp the poore out of the dung,
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 That he may set him with the princes, euen with the princes of his people.
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 He maketh the barren woman to dwell with a familie, and a ioyfull mother of children. Prayse ye the Lord.
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

< Psalms 113 >