< Psalms 109 >
1 To him that excelleth. A Psalme of David. Holde not thy tongue, O God of my praise.
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 For the mouth of the wicked, and the mouth full of deceite are opened vpon me: they haue spoken to me with a lying tongue.
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 They compassed me about also with words of hatred, and fought against me without a cause.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 For my friendship they were mine aduersaries, but I gaue my selfe to praier.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 And they haue rewarded me euil for good, and hatred for my friendship.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Set thou the wicked ouer him, and let the aduersarie stand at his right hand.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Whe he shalbe iudged, let him be condemned, and let his praier be turned into sinne.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Let his daies be fewe, and let another take his charge.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Let his children be fatherlesse, and his wife a widowe.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Let his children be vagabonds and beg and seeke bread, comming out of their places destroyed.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Let the extortioner catch al that he hath, and let the strangers spoile his labour.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 Let there be none to extend mercie vnto him: neither let there be any to shewe mercie vpon his fatherlesse children.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 Let his posteritie be destroied, and in the generation following let their name be put out.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 Let the iniquitie of his fathers bee had in remembrance with the Lord: and let not the sinne of his mother be done away.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 But let them alway be before the Lord, that he may cut off their memorial from ye earth.
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 Because he remembred not to shew mercie, but persecuted the afflicted and poore man, and the sorowfull hearted to slay him.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 As he loued cursing, so shall it come vnto him, and as he loued not blessing, so shall it be farre from him.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 As he clothed himselfe with cursing like a rayment, so shall it come into his bowels like water, and like oyle into his bones.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Let it be vnto him as a garment to couer him, and for a girdle, wherewith he shalbe alway girded.
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Let this be the rewarde of mine aduersarie from the Lord, and of them, that speake euill against my soule.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 But thou, O Lord my God, deale with me according vnto thy Name: deliuer me, (for thy mercie is good)
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 Because I am poore and needie, and mine heart is wounded within me.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 I depart like the shadowe that declineth, and am shaken off as the grashopper.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 My knees are weake through fasting, and my flesh hath lost all fatnes.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 I became also a rebuke vnto them: they that looked vpon me, shaked their heads.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Helpe me, O Lord my God: saue me according to thy mercie.
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 And they shall know, that this is thine hand, and that thou, Lord, hast done it.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Though they curse, yet thou wilt blesse: they shall arise and be confounded, but thy seruant shall reioyce.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Let mine aduersaries be clothed with shame, and let them couer themselues with their confusion, as with a cloke.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 I will giue thankes vnto the Lord greatly with my mouth and praise him among ye multitude.
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 For he will stand at the right hand of the poore, to saue him from them that woulde condemne his soule.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.