< Proverbs 28 >

1 The wicked flee when none pursueth: but the righteous are bolde as a lyon.
Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 For the transgression of the land there are many princes thereof: but by a man of vnderstanding and knowledge a realme likewise endureth long.
Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 A poore man, if he oppresse the poore, is like a raging raine, that leaueth no foode.
Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 They that forsake the Law, prayse the wicked: but they that keepe the Law, set themselues against them.
Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 Wicked men vnderstand not iudgemnt: but they that seeke the Lord vnderstand all things.
Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 Better is the poore that walketh in his vprightnesse, then hee that peruerteth his wayes, though he be riche.
Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
7 He that keepeth the Law, is a childe of vnderstanding: but hee that feedeth the gluttons, shameth his father.
Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
8 He that increaseth his riches by vsurie and interest, gathereth them for him that will be mercifull vnto the poore.
Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
9 He that turneth away his eare from hearing the Law, euen his prayer shalbe abominable.
Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
10 He that causeth the righteous to go astray by an euill way, shall fall into his owne pit, and the vpright shall inherite good things.
Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
11 The riche man is wise in his owne conceite: but the poore that hath vnderstanding, can trie him.
Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
12 When righteous men reioyce, there is great glory: but when the wicked come vp, the man is tried.
Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
13 He that hideth his sinnes, shall not prosper: but he that confesseth, and forsaketh them, shall haue mercy.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
14 Blessed is the man that feareth alway: but he that hardeneth his heart, shall fall into euill.
Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
15 As a roaring lyon, and an hungry beare, so is a wicked ruler ouer the poore people.
Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
16 A prince destitute of vnderstanding, is also a great oppressour: but hee that hateth couetousnes, shall prolong his dayes.
Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
17 A man that doeth violence against the blood of a person, shall flee vnto the graue, and they shall not stay him.
Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
18 He that walketh vprightly, shalbe saued: but he that is froward in his wayes, shall once fall.
Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
19 He that tilleth his land, shall be satisfied with bread: but he that followeth the idle, shall be filled with pouertie.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
20 A faythfull man shall abound in blessings, and he that maketh haste to be riche, shall not be innocent.
Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
21 To haue respect of persons is not good: for that man will transgresse for a piece of bread.
Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
22 A man with a wicked eye hasteth to riches, and knoweth not, that pouertie shall come vpon him.
Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
23 He that rebuketh a man, shall finde more fauour at length, then he that flattereth with his tongue.
Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
24 Hee that robbeth his father and mother, and sayth, It is no transgression, is the companion of a man that destroyeth.
Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
25 He that is of a proude heart, stirreth vp strife: but he that trusteth in the Lord, shall be fatte.
Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
26 Hee that trusteth in his owne heart, is a foole: but he that walketh in wisdome, shall be deliuered.
Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
27 He that giueth vnto the poore, shall not lacke: but he that hideth his eyes, shall haue many curses.
Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
28 When the wicked rise vp, men hide them selues: but when they perish, ye righteous increase.
Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.

< Proverbs 28 >