< Proverbs 26 >

1 As the snowe in the sommer, and as the raine in the haruest are not meete, so is honour vnseemely for a foole.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 As the sparowe by flying, and the swallow by flying escape, so the curse that is causeles, shall not come.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Vnto the horse belongeth a whip, to the asse a bridle, and a rod to the fooles backe.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Answer not a foole according to his foolishnes, least thou also be like him.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Answere a foole according to his foolishnes, least he be wise in his owne conceite.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 He that sendeth a message by the hand of a foole, is as he that cutteth off the feete, and drinketh iniquitie.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 As they that lift vp the legs of the lame, so is a parable in a fooles mouth.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 As the closing vp of a precious stone in an heape of stones, so is he that giueth glory to a foole.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 As a thorne standing vp in the hand of a drunkard, so is a parable in the mouth of fooles.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 The excellent that formed all things, both rewardeth the foole and rewardeth the transgressers.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 As a dog turneth againe to his owne vomit, so a foole turneth to his foolishnes.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Seest thou a man wise in his owne conceite? more hope is of a foole then of him.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 The slouthfull man sayth, A lyon is in the way: a lyon is in the streetes.
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 As the doore turneth vpon his hinges, so doeth the slouthfull man vpon his bed.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 The slouthfull hideth his hand in his bosome, and it grieueth him to put it againe to his mouth.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 The sluggard is wiser in his owne conceite, then seuen men that can render a reason.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 He that passeth by and medleth with the strife that belongeth not vnto him, is as one that taketh a dog by the eares.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 As he that faineth himselfe mad, casteth fire brands, arrowes, and mortall things,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 So dealeth the deceitfull man with his friend and sayth, Am not I in sport?
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Without wood the fire is quenched, and without a talebearer strife ceaseth.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 As ye cole maketh burning coles, and wood a fire, so the contentious man is apt to kindle strife.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 The wordes of a tale bearer are as flatterings, and they goe downe into the bowels of the belly.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 As siluer drosse ouerlayde vpon a potsheard, so are burning lips, and an euill heart.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 He that hateth, will counterfaite with his lips, but in his heart he layeth vp deceite.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Though he speake fauourably, beleeue him not: for there are seuen abominations in his heart.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Hatred may be couered by deceite: but the malice thereof shall be discouered in the congregation.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 He that diggeth a pit shall fall therein, and he that rolleth a stone, it shall returne vnto him.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 A false tongue hateth the afflicted, and a flattering mouth causeth ruine.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Proverbs 26 >