< Proverbs 25 >

1 THESE ARE ALSO PARABLES of Salomon, which the men of Hezekiah King of Iudah copied out.
Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2 The glorie of God is to conceale a thing secret: but the Kings honour is to search out a thing.
Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
3 The heaues in height, and the earth in deepenes, and the Kings heart can no man search out.
Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
4 Take the drosse from the siluer, and there shall proceede a vessell for the finer.
Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
5 Take away the wicked from the King, and his throne shall be stablished in righteousnes.
Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
6 Boast not thy selfe before the King, and stand not in the place of great men.
Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
7 For it is better, that it be saide vnto thee, Come vp hither, then thou to be put lower in the presece of the prince whom thine eyes haue seene.
Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
8 Goe not foorth hastily to strife, least thou know not what to doe in the ende thereof, when thy neighbour hath put thee to shame.
Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
9 Debate thy matter with thy neighbour, and discouer not the secret to another,
Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
10 Least he that heareth it put thee to shame, and thine infamie doe not cease.
au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
11 A word spoken in his place, is like apples of golde with pictures of siluer.
Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
12 He that reprooueth the wise, and the obedient eare, is as a golden earering and an ornament of fine golde.
Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
13 As the colde of the snowe in the time of haruest, so is a faithfull messenger to them that send him: for he refresheth the soule of his masters.
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
14 A man that boasteth of false liberalitie, is like cloudes and winde without raine.
Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
15 A Prince is pacified by staying of anger, and a soft tongue breaketh the bones.
Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
16 If thou haue found hony, eate that is sufficient for thee, least thou be ouerfull, and vomit it.
Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
17 Withdrawe thy foote from thy neighbours house, least he be weary of thee, and hate thee.
Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
18 A man that beareth false witnes against his neighbour, is like an hammer and a sword, and a sharpe arrowe.
Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
19 Confidence in an vnfaythfull man in time of trouble, is like a broken tooth and a sliding foote.
Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20 Hee that taketh away the garment in the colde season, is like vineger powred vpon nitre, or like him that singeth songs to an heauy heart.
Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21 If hee that hateth thee be hungry, giue him bread to eate, and if he be thirstie, giue him water to drinke.
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22 For thou shalt lay coles vpon his head, and the Lord shall recompense thee.
maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23 As the Northwinde driueth away the raine, so doeth an angry countenance the slandering tongue.
Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24 It is better to dwell in a corner of the house top, then with a contentious woman in a wide house.
Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25 As are the colde waters to a weary soule, so is good newes from a farre countery.
Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 A righteous man falling downe before the wicked, is like a troubled well, and a corrupt spring.
Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27 It is not good to eate much hony: so to search their owne glory is not glory.
Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28 A man that refraineth not his appetite, is like a citie which is broken downe and without walles.
Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.

< Proverbs 25 >