< Philippians 3 >

1 Moreouer, my brethren, reioyce in the Lord. It grieueth mee not to write the same things to you, and for you it is a sure thing.
Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
2 Beware of dogges: beware of euil workers: beware of the concision.
Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
3 For we are the circumcision, which worship God in the spirite, and reioyce in Christ Iesus, and haue no confidence in the flesh:
Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
4 Though I might also haue confidence in the flesh. If any other man thinketh that he hath whereof he might trust in the flesh, much more I,
ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
5 Circumcised the eight day, of the kinred of Israel, of the tribe of Beniamin, an Ebrewe of the Ebrewes, by the Lawe a Pharise.
Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
6 Concerning zeale, I persecuted ye Church: touching the righteousnesse which is in the Law, I was vnrebukeable.
kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
7 But the thinges that were vantage vnto me, the same I counted losse for Christes sake.
Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 Yea, doubtlesse I thinke all thinges but losse for the excellent knowledge sake of Christ Iesus my Lord, for whome I haue counted all things losse, and doe iudge them to bee dongue, that I might winne Christ,
Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
9 And might bee founde in him, that is, not hauing mine owne righteousnesse, which is of the Lawe, but that which is through the faith of Christ, euen the righteousnesse which is of God through faith,
Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
10 That I may know him, and the vertue of his resurrection, and the fellowship of his afflictions, and be made conformable vnto his death,
Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
11 If by any meanes I might attaine vnto the resurrection of the dead:
ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
12 Not as though I had alreadie attained to it, either were alreadie perfect: but I follow, if that I may comprehend that for whose sake also I am comprehended of Christ Iesus.
Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
13 Brethren, I count not my selfe, that I haue attained to it, but one thing I doe: I forget that which is behinde, and endeuour my selfe vnto that which is before,
Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
14 And follow hard toward the marke, for the prise of the hie calling of God in Christ Iesus.
Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
15 Let vs therefore as many as be perfect, be thus minded: and if yee be otherwise minded, God shall reueile euen the same vnto you.
Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
16 Neuerthelesse, in that whereunto wee are come, let vs proceede by one rule, that wee may minde one thing.
Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
17 Brethren, bee followers of mee, and looke on them, which walke so, as yee haue vs for an ensample.
Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
18 For many walke, of whom I haue told you often, and nowe tell you weeping, that they are the enemies of the Crosse of Christ:
Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
19 Whose ende is damnation, whose God is their bellie, and whose glorie is to their shame, which minde earthly things.
Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
20 But our conuersation is in heauen, from whence also we looke for the Sauiour, euen the Lord Iesus Christ,
Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
21 Who shall change our vile bodie, that it may be fashioned like vnto his glorious body, according to the working, whereby hee is able euen to subdue all things vnto him selfe.
atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.

< Philippians 3 >