< Obadiah 1 >

1 The vision of Obadiah. Thus saith the Lord God against Edom, We haue heard a rumour from the Lord, and an ambassadour is sent among the heathen: arise, and let vs rise vp against her to battel.
Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
2 Beholde, I haue made thee small among the heathen: thou art vtterly despised.
Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
3 The pride of thine heart hath deceiued thee: thou that dwellest in the cleftes of the rockes, whose habitation is hie, that saith in his heart, Who shall bring me downe to the ground?
Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
4 Though thou exalt thy selfe as the eagle, and make thy nest among the starres, thence will I bring thee downe, sayth the Lord.
Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
5 Came theeues to thee or robbers by night? howe wast thou brought to silence? woulde they not haue stolen, til they had ynough? if the grape gatherers came to thee, woulde they not leaue some grapes?
Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
6 Howe are the things of Esau sought vp, and his treasures searched?
Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
7 All the men of thy confederacie haue driuen thee to ye borders: the men that were at peace with thee, haue deceiued thee, and preuailed against thee: they that eate thy bread, haue laid a wound vnder thee: there is none vnderstanding in him.
Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
8 Shall not I in that day, saith the Lord, euen destroy the wise men out of Edom, and vnderstanding from the mount of Esau?
Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
9 And thy strong men, O Teman, shall bee afraide, because euery one of the mount of Esau shalbe cut off by slaughter.
Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
10 For thy crueltie against thy brother Iaakob, shame shall couer thee, and thou shalt be cut off for euer.
Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
11 When thou stoodest on the other side, in the day that the strangers caried away his substance, and straungers entred into his gates, and cast lots vpon Ierusalem, euen thou wast as one of them.
Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
12 But thou shouldest not haue beholden the day of thy brother, in the day that hee was made a stranger, neither shouldest thou haue reioyced ouer the children of Iudah, in the day of their destruction: thou shouldest not haue spoken proudly in the day of affliction.
Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
13 Thou shouldest not haue entred into the gate of my people, in the day of their destruction, neither shouldest thou haue once looked on their affliction in the day of their destruction, nor haue layde hands on their substance in the day of their destruction.
Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
14 Neyther shouldest thou haue stande in the crosse wayes to cut off them, that shoulde escape, neither shouldest thou haue shut vp the remnant thereof in the day of affliction.
Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
15 For the day of the Lord is neere, vpon all the heathen: as thou hast done, it shall bee done to thee: thy reward shall returne vpon thine head.
Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
16 For as yee haue drunke vpon mine holy Mountaine, so shall all the heathen drinke continually: yea, they shall drinke and swallow vp, and they shalbe as though they had not bene.
Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
17 But vpon mount Zion shalbe deliuerance, and it shalbe holy, and the house of Iaakob shall possesse their possessions,
Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
18 And the house of Iaakob shalbe a fire, and the house of Ioseph a flame, and the house of Esau as stubble, and they shall kindle in them and deuoure them: and there shall bee no remnant of the house of Esau for the Lord hath spoken it.
Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
19 And they shall possesse the South side of the mount of Esau, and the plaine of the Philistims: and they shall possesse the fieldes of Ephraim, and the fieldes of Samaria, and Beniamin shall haue Gilead.
Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
20 And the captiuitie of this host of the children of Israel, which were among the Canaanites, shall possesse vnto Zarephath, and the captiuitie of Ierusalem, which is in Sepharad, shall possesse the cities of the South.
Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
21 And they that shall saue, shall come vp to mount Zion to iudge the mount of Esau, and the kingdome shalbe the Lords.
Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.

< Obadiah 1 >