< Numbers 25 >
1 Nowe whiles Israel abode in Shittim, the people began to commit whoredome with the daughters of Moab:
Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
2 Which called the people vnto the sacrifice of their gods, and the people ate, and bowed downe to their gods.
ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
3 And Israel coupled himselfe vnto Baal Peor: wherefore the wrath of the Lord was kindled against Israel:
Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
4 And the Lord sayde vnto Moses, Take all the heades of the people, and hang them vp before the Lord against ye sunne, that the indignation of the Lords wrath may be turned from Israel.
Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
5 Then Moses sayd vnto the Iudges of Israel, Euery one slay his men that were ioyned vnto Baal Peor.
Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
6 And behold, one of the children of Israel came and brought vnto his brethren a Midianitish woman in the sight of Moses, and in the sight of all the Congregation of the children of Israel, who wept before the doore of the Tabernacle of the Congregation.
Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
7 And when Phinehas the sonne of Eleazar the sonne of Aaron the Priest sawe it, hee rose vp from the middes of the Congregation, and tooke a speare in his hand,
Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
8 And followed ye man of Israel into the tent, and thrust them both through: to wit, the man of Israel, and the woman, through her belly: so the plague ceased from the children of Israel.
akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
9 And there died in that plague, foure and twentie thousand.
Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
10 Then the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
11 Phinehas the sonne of Eleazar, the sonne of Aaron the Priest, hath turned mine anger away from the children of Israel, while hee was zealous for my sake among them: therefore I haue not consumed the children of Israel in my ielousie.
“Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
12 Wherefore say to him, Beholde, I giue vnto him my couenant of peace,
Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
13 And he shall haue it, and his seede after him, euen the couenant of the priestes office for euer, because he was zealous for his God, and hath made an atonement for the children of Israel.
Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
14 And the name of the Israelite thus slayne, which was killed with the Midianitish woman, was Zimri the sonne of Salu, prince of the familie of the Simeonites.
Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
15 And the name of the Midianitish woman, that was slayne, was Cozbi the daughter of Zur, who was head ouer the people of his fathers house in Midian.
Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
16 Againe ye Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
17 Vexe the Midianites, and smite them:
“Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
18 For they trouble you with their wiles, wherewith they haue beguiled you as concerning Peor, and as concerning their sister Cozbi ye daughter of a prince of Midian, which was slayne in the day of the plague because of Peor.
kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”