< Numbers 22 >

1 After, the children of Israel departed and pitched in the plaine of Moab on the other side of Iorden from Iericho.
Kisha Waisraeli wakasafiri katika tambarare za Moabu na kupiga kambi kando ya Mto Yordani, ngʼambo ya Yeriko.
2 Now Balak the sonne of Zippor sawe all that Israel had done to the Amorites.
Basi Balaki mwana wa Sipori, aliona mambo yale yote ambayo Israeli aliwatendea Waamori,
3 And the Moabites were sore afraide of the people, because they were many, and Moab fretted against the children of Israel.
Moabu aliogopa, kwa kuwa walikuwepo watu wengi sana. Hakika, Moabu alijawa na hofu kubwa kwa sababu ya Waisraeli.
4 Therfore Moab said vnto the Elders of Midian, Nowe shall this multitude licke vp all that are round about vs, as an oxe licketh vp ye grasse of the fielde: and Balak the sonne of Zippor was King of the Moabites at that time.
Wamoabu wakawaambia wazee wa Midiani, “Umati huu wa watu unakwenda kuramba kila kitu kinachotuzunguka, kama maksai arambavyo majani ya shambani.” Kwa hiyo Balaki mwana wa Sipori, ambaye alikuwa mfalme wa Moabu wakati huo,
5 Hee sent messengers therefore vnto Balaam the sonne of Beor to Pethor (which is by the riuer of the lande of the children of his folke) to call him, saying, Beholde, there is a people come out of Egypt, which couer the face of the earth, and lye ouer against me.
akatuma wajumbe kwenda kumwita Balaamu mwana wa Beori, ambaye alikuwa huko Pethori, karibu na Mto Frati, katika nchi yake ya kuzaliwa. Balaki akasema: “Taifa limekuja kutoka Misri, nao wamefunika uso wa nchi, nao wametua karibu nami.
6 Come now therefore, I pray thee, and curse me this people (for they are stronger then I) so it may be that I shall be able to smite them, and to driue them out of the land: for I knowe that hee, whome thou blessest, is blessed, and he whom thou cursest, shall be cursed.
Sasa uje kuwalaani watu hawa, kwa kuwa wana nguvu sana kuniliko. Kisha huenda nikaweza kuwashinda na kuwatoa nje ya nchi. Kwa kuwa ninajua kwamba, wale unaowabariki wanabarikiwa na wale unaowalaani wanalaaniwa.”
7 And the Elders of Moab, and the Elders of Midian departed, hauing the reward of the soothsaying in their hande, and they came vnto Balaam, and tolde him the wordes of Balak.
Wazee wa Moabu na wa Midiani wakaondoka, wakiwa wamechukua ada ya uaguzi. Walipokwenda kwa Balaamu, wakamweleza kile Balaki alikuwa amesema.
8 Who answered them, Tary here this night, and I will giue you an answere, as the Lord shall say vnto mee. So the princes of Moab abode with Balaam.
Balaamu akawaambia, “Mlale hapa usiku huu, nami nitawaletea jibu lile Bwana atakalonipa.” Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakakaa naye.
9 Then God came vnto Balaam, and sayde, What men are these with thee?
Mungu akamjia Balaamu na kumuuliza, “Watu gani hawa walio pamoja nawe?”
10 And Baalam said vnto God, Balak ye sonne of Zippor, king of Moab hath set vnto me, saying,
Balaamu akamwambia Mungu, “Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alinipelekea ujumbe huu:
11 Beholde, there is a people come out of Egypt and couereth the face of the earth: come nowe, curse them for my sake: so it may be that I shalbe able to ouercome them in battell, and to driue them out.
‘Taifa ambalo limekuja kutoka Misri limefunika uso wa nchi. Sasa uje unilaanie hao watu. Kisha huenda nitaweza kupigana nao na kuwafukuza.’”
12 And God said vnto Balaam, Go not thou with them, neither curse the people, for they are blessed.
Lakini Bwana akamwambia Balaamu, “Usiende pamoja nao. Hupaswi kulaani watu hao, kwa kuwa wamebarikiwa.”
13 And Balaam rose vp in the morning, and sayde vnto ye princes of Balak, Returne vnto your land: for the Lord hath refused to giue me leaue to go with you.
Asubuhi iliyofuata Balaamu akaamka, akawaambia wakuu wa Balaki, “Rudini katika nchi yenu, kwa kuwa Bwana amenikataza nisiende pamoja nanyi.”
14 So the princes of Moab rose vp, and went vnto Balak, and sayd, Balaam hath refused to come with vs.
Kwa hiyo wakuu wa Moabu wakarudi kwa Balaki na kumwambia, “Balaamu amekataa kuja pamoja nasi.”
15 Balak yet sent againe moe princes, and more honourable then they.
Kisha Balaki akatuma wakuu wengine, wengi zaidi na wanaoheshimiwa zaidi kuliko wale wa kwanza.
16 Who came to Balaam, and sayde to him, Thus saith Balak the sonne of Zippor, Bee not thou staied, I pray thee, from comming vnto me.
Wakafika kwa Balaamu na kumwambia: “Balaki mwana wa Sipori amesema hivi: Usiruhusu kitu chochote kikuzuie kuja kwangu,
17 For I wil promote thee vnto great honour, and wil do whatsoeuer thou sayest vnto me: come therefore, I pray thee, curse me this people.
kwa sababu nitakulipa vizuri sana na kufanya lolote usemalo. Njoo unilaanie watu hawa.”
18 And Balaam answered, and sayde vnto the seruants of Balak, If Balak woulde giue me his house full of siluer and golde, I can not goe beyonde the worde of the Lord my God, to doe lesse or more.
Lakini Balaamu akawajibu, “Hata kama Balaki angenipa jumba lake la kifalme likiwa limejazwa fedha na dhahabu, singeweza kufanya kitu chochote kikubwa au kidogo ili kutenda kitu nje ya agizo la Bwana Mungu wangu.
19 But nowe, I pray you, tary here this night, that I may wit, what the Lord will say vnto mee more.
Mlale hapa usiku huu kama wale wengine walivyofanya, nami nitatafuta ni nini kingine Bwana atakachoniambia.”
20 And God came vnto Balaam by night, and sayd vnto him, If the men come to call thee, rise vp, and goe with them: but onely what thing I say vnto thee, that shalt thou doe.
Usiku ule Bwana akamjia Balaamu na kumwambia, “Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita wewe, nenda nao, lakini ufanye tu lile nitakalokuambia.”
21 So Balaam rose vp early, and sadled his asse, and went with the princes of Moab.
Balaamu akaamka asubuhi, akatandika punda wake akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.
22 And ye wrath of God was kindled, because he went: and the Angel of the Lord stood in the way to be against him, as he rode vpon his asse, and his two seruants were with him.
Lakini Mungu alikasirika sana alipokwenda, naye malaika wa Bwana akasimama barabarani kumpinga. Balaamu alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.
23 And when the asse saw the Angel of the Lord stand in the way, and his sworde drawen in his hand, the asse turned out of the way and went into the field, but Balaam smote the asse, to turne her into the way.
Wakati punda alipomwona malaika wa Bwana akiwa amesimama barabarani akiwa na upanga uliofutwa mkononi mwake, punda akageukia upande kuelekea shambani. Balaamu akampiga ili amrudishe barabarani.
24 Againe the Angel of the Lord stood in a path of the vineyardes, hauing a wall on the one side, and a wall on the other.
Ndipo malaika wa Bwana akasimama katika njia nyembamba iliyo kati ya mashamba mawili ya mizabibu, yakiwa na kuta pande zote mbili.
25 And when the asse sawe the Angel of the Lord, she thrust her selfe vnto the wall, and dasht Balaams foote against the wall: wherefore hee smote her againe.
Punda alipomwona malaika wa Bwana, alijisukumiza karibu na ukuta, na kugandamiza mguu wa Balaamu ukutani. Ndipo Balaamu akampiga tena punda.
26 Then the Angel of the Lord went further, and stoode in a narowe place, where was no way to turne, either to the right hand, or to the left.
Kisha malaika wa Bwana akaendelea mbele na kusimama mahali pembamba ambapo hapakuwepo nafasi ya kugeuka, upande wa kulia wala wa kushoto.
27 And when the asse sawe the Angell of the Lord, she lay downe vnder Balaam: therefore Balaam was very wroth, and smote the asse with a staffe.
Punda alipomwona malaika wa Bwana, alilala chini Balaamu angali amempanda, naye Balaamu akakasirika na kumpiga kwa fimbo yake.
28 Then the Lord opened the mouth of the asse, and she saide vnto Balaam, What haue I done vnto thee, that thou hast smitten me nowe three times?
Kisha Bwana akakifungua kinywa cha punda, akamwambia Balaamu, “Nimekutendea nini kinachokufanya unipige mara hizi tatu?”
29 And Balaam saide vnto the asse, Because thou hast mocked me: I woulde there were a sworde in mine hand, for nowe would I kill thee.
Balaamu akamjibu punda, “Umenifanya mjinga! Kama ningelikuwa na upanga mkononi mwangu, ningelikuua sasa hivi.”
30 And the asse saide vnto Balaam, Am not I thine asse, which thou hast ridden vpon since thy first time vnto this day? haue I vsed at any time to doe thus vnto thee? Who said, Nay.
Punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako mwenyewe, ambaye umenipanda siku zote, hadi leo? Je, nimekuwa na tabia ya kufanya hivi kwako?” Akajibu, “Hapana.”
31 And the Lord opened the eyes of Balaam, and he sawe the Angel of the Lord standing in the way with his sword drawen in his hande: then he bowed him selfe, and fell flat on his face.
Kisha Bwana akafungua macho ya Balaamu, naye akamwona malaika wa Bwana amesimama barabarani akiwa ameufuta upanga wake. Balaamu akainama, akaanguka kifudifudi.
32 And the Angel of the Lord said vnto him, Wherefore hast thou nowe smitten thine asse three times? beholde, I came out to withstande thee, because thy way is not straight before me.
Malaika wa Bwana akamuuliza Balaamu, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu hizi? Nimekuja kukuzuia kwa sababu njia yako imepotoka mbele yangu.
33 But the asse sawe me, and turned from me now three times: for els, if she had not turned from me, surely I had euen nowe slaine thee, and saued her aliue.
Punda aliniona na kunikwepa mara hizi tatu. Kama punda hangenikwepa, hakika ningekuwa nimeshakuua sasa, lakini ningemwacha punda hai.”
34 Then Balaam saide vnto the Angel of the Lord, I haue sinned: for I wist not that thou stoodest in the way against me: now therefore if it displease thee, I will turne home againe.
Balaamu akamwambia malaika wa Bwana, “Nimetenda dhambi. Sikutambua kuwa umesimama barabarani kunizuia. Basi kama haikupendezi, nitarudi.”
35 But the Angel said vnto Balaam, Go with the men: but what I say vnto thee, that shalt thou speake. So Balaam went with ye princes of Balak.
Malaika wa Bwana akamwambia Balaamu, “Uende na watu hao, lakini useme tu lile nikuambialo.” Kwa hiyo Balaamu akaenda na wale wakuu wa Balaki.
36 And when Balak heard that Balaam came, he went out to meete him vnto a citie of Moab, which is in the border of Arnon, euen in the vtmost coast.
Balaki aliposikia kuwa Balaamu anakuja, akatoka kumlaki katika mji wa Moabu, katika mpaka wa Arnoni, ukingoni mwa nchi yake.
37 Then Balak saide vnto Balaam, Did I not sende for thee to call thee? Wherefore camest thou not vnto me? am I not able in deede to promote thee vnto honour?
Balaki akamwambia Balaamu, “Je, sikukupelekea jumbe za haraka? Kwa nini hukuja kwangu? Hivi kweli mimi siwezi kukulipa?”
38 And Balaam made answere vnto Balak, Lo, I am come vnto thee, and can I nowe say any thing at all? the worde that God putteth in my mouth, that shall I speake.
Balaamu akajibu, “Vema, sasa nimekuja kwako. Lakini kwani nina uwezo wa kusema tu chochote? Ni lazima niseme tu kile ambacho Mungu ataweka kinywani mwangu.”
39 So Balaam went with Balak, and they came vnto the citie of Huzoth.
Kisha Balaamu alikwenda na Balaki mpaka Kiriath-Husothi.
40 Then Balak offred bullockes, and sheepe, and sent thereof to Balaam, and to the princes that were with him.
Balaki akatoa dhabihu ya ngʼombe na kondoo; baadhi yake akampa Balaamu na wakuu waliokuwa pamoja naye.
41 And on the morowe Balak tooke Balaam, and brought him vp into the hie places of Baal, that thence hee might see the vtmost part of the people.
Asubuhi iliyofuata Balaki akamchukua Balaamu mpaka Bamoth-Baali, na kutoka huko Balaamu akawaona baadhi ya watu.

< Numbers 22 >