< Numbers 15 >

1 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
2 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, Whe ye be come into the land of your habitations, which I giue vnto you,
“Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
3 And will make an offring by fire vnto the Lord, a burnt offring or a sacrifice to fulfil a vowe, or a free offring, or in your feastes, to make a sweete sauour vnto the Lord of the hearde, or of the flocke.
mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
4 Then let him that offreth his offring vnto the Lord, bring a meate offring of a tenth deale of fine flowre, mingled with the fourth part of an Hin of oyle.
Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
5 Also thou shalt prepare ye fourth part of an Hin of wine to be powred on a lambe, appointed for the burnt offring or any offring.
Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
6 And for a ram, thou shalt for a meat offring, prepare two tenth deales of fine floure, mingled with the third part of an Hin of oyle.
Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
7 And for a drinke-offering, thou shalt offer the third part of an Hin of wine, for a sweete sauour vnto the Lord.
Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
8 And when thou preparest a bullocke for a burnt offring, or for a sacrifice to fulfill a vowe or a peace offring to the Lord,
Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
9 Then let him offer with ye bullocke a meate offring of three tenth deales of fine floure, mingled with halfe an Hin of oyle.
Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
10 And thou shalt bring for a drinke offring halfe an Hin of wine, for an offring made by fire of a sweete sauour vnto the Lord.
Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
11 Thus shall it be done for a bullocke, or for a ram, or for a lambe, or for a kid.
Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
12 According to the nomber that yee prepare to offer, so shall yee doe to euery one according to their nomber.
Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
13 All that are borne of the countrey, shall do these things thus, to offer an offring made by fire of sweete sauour vnto the Lord.
Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
14 And if a stranger soiourne with you, or whosoeuer bee among you in your generations, and will make an offring by fire of a sweete sauour vnto the Lord, as ye do, so hee shall doe.
Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
15 One ordinance shalbe both for you of the Congregation, and also for the stranger that dwelleth with you, euen an ordinance for euer in your generations: as you are, so shall the stranger bee before the Lord.
Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
16 One Lawe and one maner shall serue both for you and for the stranger that soiourneth with you.
Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
17 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
18 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, When ye be come into the lande, to the which I bring you,
“Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
19 And when ye shall eate of the bread of the land, ye shall offer an heaue offring vnto ye Lord.
mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
20 Ye shall offer vp a cake of the first of your dowe for an heaue offring: as the heaue offring of the barne, so ye shall lift it vp.
Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
21 Of the first of your dowe ye shall giue vnto the Lord an heaue offring in your generations.
Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
22 And if ye haue erred, and not obserued all these commandements, which the Lord hath spoken vnto Moses,
Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
23 Euen all that the Lord hath commanded you by the hand of Moses, from the first day that the Lord commanded Moses, and hence forward among your generations:
-kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
24 And if so be that ought be committed ignorantly of the Congregation, then all ye Congregatio shall giue a bullocke for a burnt offring, for a sweete sauour vnto the Lord, with the meat offring and drinke offring thereto, according to the maner, and an hee goate for a sinne offring.
Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
25 And the Priest shall make an atonement for al the Congregation of the children of Israel, and it shalbe forgiuen them: for it is ignorance: and they shall bring their offring for an offring made by fire vnto the Lord, and their sinne offering before the Lord for their ignorance.
Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
26 Then it shalbe forgiuen all the Congregation of the children of Israel, and the stranger that dwelleth among them: for all the people were in ignorance.
Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
27 But if any one person sinne through ignorance, then he shall bring a shee goate of a yeere olde for a sinne offring.
Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
28 And the Priest shall make an atonement for the ignorant person, when hee sinneth by ignorance before the Lord, to make reconciliation for him: and it shalbe forgiuen him.
Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
29 He that is borne among the children of Israel, and the stranger that dwelleth among them, shall haue both one lawe, who so doth sinne by ignorance.
Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
30 But the person that doeth ought presumptuously, whether he be borne in the land, or a stranger, the same blasphemeth the Lord: therefore that person shalbe cut off from among his people,
Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
31 Because he hath despised the worde of the Lord, and hath broken his commandement: that person shalbe vtterly cut off: his iniquitie shalbe vpon him.
Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
32 And while the children of Israel were in the wildernesse, they found a man that gathered stickes vpon the Sabbath day.
Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
33 And they that found him gathering sticks, brought him vnto Moses and to Aaron, and vnto all the Congregation,
Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
34 And they put him warde: for it was not declared what should be done vnto him.
Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
35 Then the Lord said vnto Moses, This man shall dye the death: and let al the multitude stone him with stones without the hoste.
Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
36 And all the Congregation brought him without the hoste, and stoned him with stones, and he died, as the Lord had commanded Moses.
Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
37 And the Lord spake vnto Moses, saying,
BWANA akanena na Musa tena, akasema,
38 Speake vnto the children of Israel, and bid them that they make them fringes vpon the borders of their garments throughout their generations, and put vpon the fringes of the borders a ryband of blewe silke.
“Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
39 And ye shall haue the fringes, that when ye looke vpon them, ye may remember all the commandemets of the Lord, and do them: and that ye seeke not after your own heart, nor after your owne eyes, after the which ye go a whoring;
Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
40 That yee may remember and doe all my commandements, and bee holy vnto your God.
Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
41 I am the Lord your God, which brought you out of the lande of Egypt, to bee your God: I am the Lord your God.
Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”

< Numbers 15 >