< Numbers 15 >

1 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, Whe ye be come into the land of your habitations, which I giue vnto you,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
3 And will make an offring by fire vnto the Lord, a burnt offring or a sacrifice to fulfil a vowe, or a free offring, or in your feastes, to make a sweete sauour vnto the Lord of the hearde, or of the flocke.
nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
4 Then let him that offreth his offring vnto the Lord, bring a meate offring of a tenth deale of fine flowre, mingled with the fourth part of an Hin of oyle.
ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
5 Also thou shalt prepare ye fourth part of an Hin of wine to be powred on a lambe, appointed for the burnt offring or any offring.
Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
6 And for a ram, thou shalt for a meat offring, prepare two tenth deales of fine floure, mingled with the third part of an Hin of oyle.
“‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
7 And for a drinke-offering, thou shalt offer the third part of an Hin of wine, for a sweete sauour vnto the Lord.
na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
8 And when thou preparest a bullocke for a burnt offring, or for a sacrifice to fulfill a vowe or a peace offring to the Lord,
“‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
9 Then let him offer with ye bullocke a meate offring of three tenth deales of fine floure, mingled with halfe an Hin of oyle.
leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
10 And thou shalt bring for a drinke offring halfe an Hin of wine, for an offring made by fire of a sweete sauour vnto the Lord.
Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
11 Thus shall it be done for a bullocke, or for a ram, or for a lambe, or for a kid.
Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
12 According to the nomber that yee prepare to offer, so shall yee doe to euery one according to their nomber.
Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
13 All that are borne of the countrey, shall do these things thus, to offer an offring made by fire of sweete sauour vnto the Lord.
“‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
14 And if a stranger soiourne with you, or whosoeuer bee among you in your generations, and will make an offring by fire of a sweete sauour vnto the Lord, as ye do, so hee shall doe.
Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
15 One ordinance shalbe both for you of the Congregation, and also for the stranger that dwelleth with you, euen an ordinance for euer in your generations: as you are, so shall the stranger bee before the Lord.
Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
16 One Lawe and one maner shall serue both for you and for the stranger that soiourneth with you.
Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
17 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
18 Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, When ye be come into the lande, to the which I bring you,
“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
19 And when ye shall eate of the bread of the land, ye shall offer an heaue offring vnto ye Lord.
nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
20 Ye shall offer vp a cake of the first of your dowe for an heaue offring: as the heaue offring of the barne, so ye shall lift it vp.
Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
21 Of the first of your dowe ye shall giue vnto the Lord an heaue offring in your generations.
Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
22 And if ye haue erred, and not obserued all these commandements, which the Lord hath spoken vnto Moses,
“‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
23 Euen all that the Lord hath commanded you by the hand of Moses, from the first day that the Lord commanded Moses, and hence forward among your generations:
amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
24 And if so be that ought be committed ignorantly of the Congregation, then all ye Congregatio shall giue a bullocke for a burnt offring, for a sweete sauour vnto the Lord, with the meat offring and drinke offring thereto, according to the maner, and an hee goate for a sinne offring.
ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
25 And the Priest shall make an atonement for al the Congregation of the children of Israel, and it shalbe forgiuen them: for it is ignorance: and they shall bring their offring for an offring made by fire vnto the Lord, and their sinne offering before the Lord for their ignorance.
Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
26 Then it shalbe forgiuen all the Congregation of the children of Israel, and the stranger that dwelleth among them: for all the people were in ignorance.
Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
27 But if any one person sinne through ignorance, then he shall bring a shee goate of a yeere olde for a sinne offring.
“‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
28 And the Priest shall make an atonement for the ignorant person, when hee sinneth by ignorance before the Lord, to make reconciliation for him: and it shalbe forgiuen him.
Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
29 He that is borne among the children of Israel, and the stranger that dwelleth among them, shall haue both one lawe, who so doth sinne by ignorance.
Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
30 But the person that doeth ought presumptuously, whether he be borne in the land, or a stranger, the same blasphemeth the Lord: therefore that person shalbe cut off from among his people,
“‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
31 Because he hath despised the worde of the Lord, and hath broken his commandement: that person shalbe vtterly cut off: his iniquitie shalbe vpon him.
Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
32 And while the children of Israel were in the wildernesse, they found a man that gathered stickes vpon the Sabbath day.
Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
33 And they that found him gathering sticks, brought him vnto Moses and to Aaron, and vnto all the Congregation,
Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
34 And they put him warde: for it was not declared what should be done vnto him.
nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
35 Then the Lord said vnto Moses, This man shall dye the death: and let al the multitude stone him with stones without the hoste.
Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
36 And all the Congregation brought him without the hoste, and stoned him with stones, and he died, as the Lord had commanded Moses.
Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
37 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
38 Speake vnto the children of Israel, and bid them that they make them fringes vpon the borders of their garments throughout their generations, and put vpon the fringes of the borders a ryband of blewe silke.
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
39 And ye shall haue the fringes, that when ye looke vpon them, ye may remember all the commandemets of the Lord, and do them: and that ye seeke not after your own heart, nor after your owne eyes, after the which ye go a whoring;
Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
40 That yee may remember and doe all my commandements, and bee holy vnto your God.
Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
41 I am the Lord your God, which brought you out of the lande of Egypt, to bee your God: I am the Lord your God.
Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”

< Numbers 15 >