< Nehemiah 8 >

1 And all the people assembled themselues together, in the streete that was before the watergate, and they spake vnto Ezra the Scribe, that hee would bring the booke of ye Law of Moses, which the Lord had commanded to Israel.
watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Sheria ya Mose, ambacho Bwana aliamuru kwa ajili ya Israeli.
2 And Ezra the Priest brought the Lawe before the Congregation both of men and women, and of all that coulde heare and vnderstand it, in the first day of the seuenth moneth,
Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
3 And he read therein in the streete that was before the watergate (from the morning vntill the midday) before men and women, and them that vnderstoode it, and the eares of all the people hearkened vnto the booke of the Lawe.
Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko mpaka adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Sheria.
4 And Ezra the Scribe stoode vpon a pulpit of wood which he had made for the preaching, and beside him stood Mattithiah, and Shema, and Ananiah, and Vriiah, and Hilkiah, and Maaseiah on his right hande, and on his left hand Pedaiah, and Mishael, and Malchiah, and Hashum, and Hashbadana, Zechariah, and Meshullam.
Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume alisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwepo Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
5 And Ezra opened the booke before all the people: for hee was aboue all the people: and when he opened it, all the people stoode vp.
Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
6 And Ezra praysed the Lord the great God, and all the people answered, Amen, Amen, with lifting vp their handes: and they bowed themselues, and worshipped the Lord with their faces toward the grounde.
Ezra akamsifu Bwana, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Bwana hali nyuso zao zikigusa ardhi.
7 Also Ieshua, and Bani, and Sherebiah, Iamin, Akkub, Shabbethai, Hodiiah, Maaseiah, Kelita, Azariah, Iozabad, Hanan, Pelaiah, and the Leuites caused the people to vnderstand the lawe, and the people stood in their place.
Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafunza ile Sheria: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
8 And they read in the booke of the Lawe of God distinctly, and gaue the sense, and caused them to vnderstand the reading.
Walisoma kutoka kile Kitabu cha Sheria ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
9 Then Nehemiah (which is Tirshatha) and Ezra the Priest and scribe, and the Leuites that instructed the people, saide vnto all the people, This day is holie vnto ye Lord your God: mourne not, neither weepe: for all the people wept, whe they heard the words of the Lawe.
Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Sheria.
10 He saide also vnto the, Go, and eate of the fat, and drinke the sweete, and send part vnto them, for whome none is prepared: for this day is holie vnto our Lord: be ye not sorie therefore: for the ioy of the Lord is your strength.
Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”
11 And the Leuites made silence throughout all the people, saying, Holde your peace: for the day is holy, be not sad therefore.
Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
12 Then all the people went to eate and to drinke, and to send away part, and to make great ioy, because they had vnderstand the wordes that they had taught them.
Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
13 And on the second day the chiefe fathers of all the people, the Priests and the Leuites were gathered vnto Ezra the scribe, that he also might instruct them in the wordes of the Lawe.
Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa mbari zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Sheria.
14 And they found written in the Law, (that the Lord had commanded by Moses) that the children of Israel should dwel in boothes in the feast of the seuenth moneth,
Wakakuta imeandikwa katika ile Sheria, ambayo Bwana aliiamuru kupitia kwa Mose, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
15 And that they shoulde cause it to bee declared and proclaimed in all their cities, and in Ierusalem, saying, Go forth vnto the mount, and bring oliue branches, and pine branches, and branches of myrtus, and palme branches, and branches of thicke trees, to make boothes, as it is written.
na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Enendeni katika nchi ya mlima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
16 So the people went foorth and brought them, and made them boothes, euerie one vpon the roofe of his house, and in their courtes, and in the courtes of the house of God, and in the streete by the watergate, and in the streete of the gate of Ephraim.
Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji na uwanja wa Lango la Efraimu.
17 And all the Congregation of them that were come againe out of the captiuitie made boothes, and sate vnder the boothes: for since the time of Ieshua the sonne of Nun vnto this day, had not the children of Israel done so, and there was very great ioy.
Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni mpaka siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
18 And he read in the booke of the Lawe of God euery day, from the first day vnto the last day. and they kept the feast seuen dayes, and on the eight day a solemne assemblie, according vnto the maner.
Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.

< Nehemiah 8 >