< Nehemiah 12 >

1 These also are the Priestes and the Leuites that went vp with Zerubbabel, the sonne of Shealtiel, and Ieshua: to wit, Seraiah, Ieremiah, Ezra,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amariah, Malluch, Hattush,
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Shecaniah, Rehum, Merimoth,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Iddo, Ginnetho, Abiiah,
Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Miamin, Maadiah, Bilgah,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Shemaiah, and Ioiarib, Iedaiah,
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Sallu, Amok, Hilkiiah, Iedaiah: these were the chiefe of the Priests, and of their brethren in the dayes of Ieshua.
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 And the Leuites, Ieshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Iudah, Mattaniah were ouer the thankesgiuings, he, and his brethren.
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 And Bakbukiah and Vnni, and their brethren were about them in the watches.
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 And Ieshua begate Ioiakim: Ioiakim also begate Eliashib, and Eliashib begate Ioiada.
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 And Ioiada begate Ionathan, and Ionathan begate Iaddua,
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 And in the daies of Ioiakim were these, the chiefe fathers of the Priests: vnder Seraiah was Meraiah, vnder Ieremiah, Hananiah,
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 Vnder Ezra, Meshullam, vnder Amariah, Iehohanan,
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 Vnder Melicu, Ionathan, vnder Shebaniah, Ioseph,
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 Vnder Harim, Adna, vnder Maraioth, Helkai,
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 Vnder Iddo, Zechariah, vnder Ginnithon, Meshullam,
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 Vnder Abiiah, Zichri, vnder Miniamin, and vnder Moadiah, Piltai,
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 Vnder Bilgah, Shammua, vnder Shemaiah, Iehonathan,
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 Vnder Ioiarib, Mattenai, vnder Iedaiah, Vzzi,
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 Vnder Sallai, Kallai, vnder Amok, Eber,
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 Vnder Hilkiah, Hashabiah, vnder Iedaiah, Nethaneel.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 In the dayes of Eliashib, Ioiada, and Iohanan and Iaddua were the chiefe fathers of the Leuites written, and the Priests in the reigne of Darius the Persian.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 The sonnes of Leui, the chiefe fathers were written in the booke of the Chronicles euen vnto the dayes of Iohanan the sonne of Eliashib.
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 And the chiefe of the Leuites were Hashabiah, Sherebiah, and Ieshua the sonne of Kadmiel, and their brethren about them to giue prayse and thankes, according to the ordinance of Dauid the man of God, ward ouer against warde.
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 Mattaniah and Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon and Akkub were porters keeping the warde at the thresholds of the gates.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 These were in the dayes of Ioiakim, the sonne of Ieshua, the sonne of Iozadak, and in the dayes of Nehemiah the captaine, and of Ezra the Priest and scribe.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 And in the dedication of the wall at Ierusalem they sought the Leuites out of all their places to bring them to Ierusalem to keepe the dedication and gladnes, both with thankesgiuings and with songs, cymbales, violes and with harpes.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 Then the singers gathered themselues together both from the plaine countrey about Ierusalem, and from the villages of Netophathi,
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 And from the house of Gilgal, and out of the countreis of Geba, and Azmaueth: for the singers had built them villages round about Ierusalem.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 And the Priests and Leuites were purified, and clensed the people, and the gates, and the wall.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 And I brought vp the princes of Iudah vpon the wall, and appointed two great companies to giue thankes, and the one went on the right hand of the wall toward the dung gate.
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 And after them went Hoshaiah, and halfe of the princes of Iudah,
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 And Azariah, Ezra and Meshullam,
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Iudah, Beniamin, and Shemaiah, and Ieremiah,
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 And of the Priests sonnes with trumpets, Zechariah the sonne of Ionathan, the sonne of Shemaiah, the sonne of Mattaniah, the sonne of Michaiah, the sonne of Zaccur, ye sonne of Asaph.
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 And his brethren, Shemaiah, and Azareel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneel, and Iudah, Hanani, with the musicall instruments of Dauid the man of God: and Ezra the scribe went before them.
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 And to the gate of the fountaine, euen ouer against them went they vp by the staires of the citie of Dauid, at the going vp of the wall beyond the house of Dauid, euen vnto the water gate Eastward.
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 And the seconde companie of them that gaue thankes, went on the other side, and I after them, and the halfe of the people was vpon the wall, and vpon the towre of the furnaces euen vnto the broad wall.
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 And vpon the gate of Ephraim, and vpon the olde gate, and vpon the fishgate, and the towre of Hananeel, and the towre of Meah, euen vnto the sheepegate: and they stood in the gate of the warde.
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 So stood the two companies (of them that gaue thankes) in the house of God, and I and the halfe of the rulers with me.
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 The Priests also, Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Michaiah, Elioenai, Zechariah, Hananiah, with trumpets,
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 And Maaseiah, and Shemaiah, and Eleazar, and Vzzi, and Iehohanan, and Malchiiah, and Elam, and Ezer: and the singers sang loude, hauing Izrahiah which was the ouerseer.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 And the same day they offered great sacrifices and reioyced: for God had giuen them great ioy, so that both the women, and the children were ioyfull: and the ioy of Ierusalem was heard farre off.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Also at the same time were men appointed ouer the chambers of the store for the offerings (for the first fruites, and for the tithes) to gather into them out of the fieldes of the cities, the portions of the Law for the Priests and the Leuites: for Iudah reioyced for the Priests and for the Leuites, that serued.
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 And both the singers and the Leuites kept the ward of their God, and the warde of the purification according to the commandement of Dauid, and Salomon his sonne.
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 For in the dayes of Dauid and Asaph, of olde were chiefe singers, and songs of praise and thankesgiuing vnto God.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 And in the dayes of Zerubbabel, and in the dayes of Nehemiah did al Israel giue portions vnto the singers and porters, euerie day his portion, and they gaue the holy things vnto the Leuites, and the Leuites gaue the holy things vnto the sonnes of Aaron.
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

< Nehemiah 12 >